Katibu wa bakwata Mkoa wa Arusha Bw. Abdulkarimu Jonjo akiugulia maumivu katika wodi ya majeruhi ,katika hospitali ya mkoa mount Meru baada ya kulipuliwa na bomu la kutupwa na mkono akiwa amelala usingizini nyumbani kwake na watu wasiofahamika majira ya saa 6.30 usiku wa kuamkia leo. Picha na Josefu Ngilisho.
KATIBU
mkuu wa Bakwata mkoani Arusha,Abdulkarim Jonjo (52) mkazi wa Esso
jijini Arusha,amenusulika kufa baada ya kujeruhiwa vibaya na kulazwa
katika hospital ya Mkoa Mount Meru baada ya watu wasiojulikana kumlipua
kwa bomu la kurushwa kwa mkono akiwa amelala usingizini nyumbani kwake.
Akiongea kwa taabu katika wodi ya majeruhi hospitalini hapo,Jonjo alisema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa 6.30 usiku akiwa amelala baada ya kuona mwanga wa cheche dirishani kwake na kufuatiwa na kishindo cha mlipuko.
Alisema kuwa hali hiyo ilimlazimu kuinuka kitandani kuangalia tukio la mwanga huo wa cheche,lakini kabla ya kuufikia alisikia kishindo cha mlipuko mkubwa kilichosababisha kujeruhiwa vibaya baada ya kurushwa umbali ndani ya chumba chake.
‘’unajua jana nilichelewa kulala kutokana na umeme kukatika nilikaa sebuleni hadi saa 5 kasoro dakika 20 nikaenda kulala ,lakini ilipofika majira ya saa 6 kasorobo niliamka kuchaji simu yangu baada ya kuona umeme umerudi na kwenda kulala ,ila ilipofika saa 6.30 ndipo nilisikia cheche dirishani na kufuatiwa na mlipuko’’alisema Jonjo.
Akiongea kwa taabu katika wodi ya majeruhi hospitalini hapo,Jonjo alisema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa 6.30 usiku akiwa amelala baada ya kuona mwanga wa cheche dirishani kwake na kufuatiwa na kishindo cha mlipuko.
Alisema kuwa hali hiyo ilimlazimu kuinuka kitandani kuangalia tukio la mwanga huo wa cheche,lakini kabla ya kuufikia alisikia kishindo cha mlipuko mkubwa kilichosababisha kujeruhiwa vibaya baada ya kurushwa umbali ndani ya chumba chake.
‘’unajua jana nilichelewa kulala kutokana na umeme kukatika nilikaa sebuleni hadi saa 5 kasoro dakika 20 nikaenda kulala ,lakini ilipofika majira ya saa 6 kasorobo niliamka kuchaji simu yangu baada ya kuona umeme umerudi na kwenda kulala ,ila ilipofika saa 6.30 ndipo nilisikia cheche dirishani na kufuatiwa na mlipuko’’alisema Jonjo.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus SABAS ameapa kuwasaka waliohusika na
tukio hilo linalofananishwa na ugaidi na kuwafikisha mahakamani.
No comments:
Post a Comment