Shiliningi milioni 5 za kitanzania zinahitajika ili kuwanusuru watu wawili walionasiana wakivunja amri sita.
Watu
wawili wakazi wa jijini Dar es Salaam wanadaiwa kukutwa wakiwa
wamenasana wakati wakifanya tendo maalum la watu walio katika mahusiano
(mke na mume) na kwakua wao sio mke na mume halali wamenasiana.
Mume
wa mwanake ambae amefikwa na maswaibu hayo ya mwaka jijini Dar es
Salaam anahitaji kiasi hicho cha fedha ili atoe PASSWORD ya pin hiyo
kali aliuyoiweka katika eneo takatifu la unyumba wao.
Taarifa
za awali kutoka Temeke zinapasha kuwa wawili hao wapo katika hospitali
ya Temeke jijini Dar es Salaam kwa unasuaji ambao wadadisi wa mambo hasa
ya kijamii wanadai Hospitali hawataweza kuwanasua isipokuwa kwa wataalm
wa jadi hasa Mume wa Mwenye mke ambaye aliwekewa tego.
Blog
hii itatujuza zaidi juu ya tukio hilo ambalo hadi sasa limekuwa ni
gumzo jijini na kujaza umati mkubwa wa watu na kusababisha polisi
kutumia mabomu ya machozi kutawanya watu eneo la tukio.
UMATI
wa watu wakiwa wamefurika katika Hospitali ya Temeke, Dar es Salaam ,
mapema leo wakiwa na hamu ya kutaka kuwaona mwanaume na mke wa mtu
waliodaiwa kugandiana wakifanya mapenzi katika moja ya nyumba za kulala
wageni wilayani Temeke.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Temeke, Dk. Aman Malima akishangaa kuona umati huo
Police walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu waliofurika Hospitali ya Temeke kushudia tukio hilo
Baadhi ya watu wakiwa hapo kushudia watu hao walio gandiana
Wananchi wakishinikiza waoneshwe wapenzi hao