Blogger Widgets

December 15, 2012

Ya Wakubwa Watoto kulala:Jua mambo saba yakutilia maanani kabla ya Kukutana na Mpenzi wako kwenye sita kwa sita


 

1. LAZIMA UJUE  MADHARA YA KUJAMIIANA:Mimba ni  suala la kwanza kulifikiria.Lakini  kumbuka pia kuna magonjwa mengi sana  yatokanayo  na kufanya  mapenzi kama zinaa  na UKIMWI.

2. UWE  NA NJIA MBADALA  YA  KUPAMBANA NA HAYO  MADHARA:  Ongea  na mpenzi wako uone kama  yuko tayari kutumia Kondom  na  Vidonge.Kamahayuko tayari,kuwa huru  kufanya  maamuzi sahihi.

3.
MMEJIPANGA VIPI  ENDAPO MTAPATA MIMBA?: Hata ungekuwa  makini kivipi, ukweli nikwamba  kondom nimuhimu sana hasa ikiwa hamko tayari  kuwa wazazi kwa wakati huo .

4.
HAKIKISHA UNA MIAKA  18 NAKUENDELEA: Kama hujafikisha miaka 18  nakushaur usithubutu  kujihusisha  na mambo  ya mapenzi kwa sababu viungo vyako bado haviko tayari.Kujiingiiza katika mapenzi katika umri mdogo ni  kujiharibia  mfumo wako wa uzazi na  kujijengea msingi wa kuwa tasa.Kumbuka sharia ziliwekwa makusudi ili zikusaidie wewe.

5.USIKUBALI KUFANYA MAAMUZI UKIWA UMELEWA.: Pombe haimuongozi mtu kufanya maamuzi sahihi.Epuka kufanya  maamuzi yatakayo  kufanya ujute maishani,tena kwa raha ya masaa machache tu..

 6. MWAMINI MPENZI WAKO: Mimi naamini  kuwa mpaka mtuunafikia hatua ya kumvulia mtu nguo ni kwamba una mwamini kweli kweli.Usikurupe.Tambua thamani ya mwili wako na kumbuka kuwa mapenzi hayalazimishi.Wengi waliolazimisha penzi waliishia kujuta na kujiua.

7.
KUWA TAYARI KWA  LOLOTE:Inawezekana kabisa ulichokuwa unakitegemea kwa mpenzi wako hukipati.Yawezekana akawa hajui mapenzi,si mbunifu au hakufikishi.Suluhu si kukimbia tatizo bali ni kutafuta jinsi ya kutatua .