Desturi ya kuvaa nguo kali na za gharama muda wote haitegemei uwezo peke yake bali moyo na utayari wa mtu kuwa muumini wa uvaaji pamba kali. Kuna mastaa kibao nchini ambao licha ya kuwa na uwezo mzuri wa kifedha wameendelea kuvaa kawaida tu (si jambo baya sababu ni uamuzi binafsi).
Lakini wapo wasanii ambao wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kujiweka katika utanashati wa hali ya juu kwa kuvaa nguo kali na za gharama. Japokuwa wanaweza kuwepo wengine, hawa ni miongoni mwa wasanii wa Tanzania wanaopiga pamba kali zaidi kwa mujibu wa Bongo5.
1. Jux
2. Hemedy
3. Cyril
4. Bob Junior
5. Gelly wa Rhymes
6. Izzo B
7. Diamond