Wasamariawema
wakimsafisha uchafu mtoto mchanga baada ya kumuokota katika eneo la
bondeni huko Kimara Baruti Bondeni karibu na maeneo ya Ubungo Kibangu.
Leo
asubuhi wasamaria wema wamekiokota kitoto kichanga cha
kiume huko Kimara baruti bondeni karibu na Ubungo kibangu , wasamaria
hao baada ya kumsafisha uchafu na damu waliamua kumpeleka mtoto huyo
kwenye hospital ya Palestina kwa huduma ya kwanza na baadae Hospital ya
Mwananyamala ambako kuna kitengo maalumu cha kuhudumia watoto
wachanga . Baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa kuna
uwezekano wa mtoto huyo kutupwa leo asubuhi na hii imetokana na mtoto
huyo kukutwa akiwa hai na uwepo wa damu mbichi mwilini mwake
Respect:Chinga