Blogger Widgets

March 6, 2013

Hii Ndio List ya Wasanii 11 wa Kike waliopata Bahati ya Kuhit sana kwa 2013

1. Jokate Mwegelo 
 
Mrembo huyu anafahamika pia kwa jina la Kidoti – jina ambalo limeanzisha kampuni yake ya fashion yenye jina hilo. Ni mshiriki wa Miss Tanzania, mbunifu wa mitindo, mtangazaji na msanii pia wa muziki. Hajawahi kutoa wimbo wake mwenyewe zaidi ya kushirikishwa tu. Alianza kusikika kwenye ngoma ya AY King and Queens. Mwaka jana alishirikishwa kwenye albam ya Kala Jeremiah, Pasaka na pia mwaka huu amesikika kwenye ngoma ya Lucci ‘Waters Up’ Kuna project zake kadhaa pia kwenye studio za TransformaX ambazo hazijatoka.
2. Nuru the Light

IMG_5048

Nuru Magram aka Nuru the Light ni blogger na mwanamuziki aishie Stockholm, Sweden. Pamoja na kupenda fashion, Nuru amekuwa akirudi Tanzania na kutengeneza ngoma kadhaa zikiwemo ‘Muhogo Andazi’ aliomshirikisha Bob Junior, Chapa Lapa na zingine.
3. Feza Kessy

62463_10152632992750473_172344653_n

Feza Kessy ni msanii mpya aliye chini ya usimamizi wa kampuni ya AY, Unity Entertaiment. Mwezi uliopita aliachia single yake ya kwanza iitwayo Amani ya Moyo na ambayo inafanya vizuri kwa sasa. Tangu aachie wimbo wake wa kwanza, mrembo huyu aliyewahi kushikilia taji la Miss Dar City Centre amewathibitishia watanzania kuwa si kwamba kabarikiwa uzuri tu bali pia sauti tamu ya kuimba.
4. Zuhura
Zuhura_crop
Zuhuru Mrisho si msanii maarufu sana nchini licha ya kuwepo kwa muda sasa. Aliwahi kushika taji la Nokia Face of Africa 2006, lililomjumuisha kwenye ramani za mastaa wa Bongo. Mrembo huyo aliyepitia nyumba ya vipaji ya THT, alitambulishwa kwenye game ya muziki kupitia wimbo wenye jina la Limupenzi, na Shida na Raha aliyompa shavu Banana na mpaka sasa ana albam moja. Kwa sasa ana video mpya ya wimbo wake Songesha.
5. Menynah Atick
301064_432818613431794_2048813241_n
Menynah ni mshiriki wa shindano la Bongo Star Search mwaka jana na ambaye aliingia kwenye shindano hilo kwa usaili wa njia ya simu. Ni msichana mdogo ambaye baada ya shindano hilo kumalizika ameachia wimbo uitwao ‘Dream Tonight’. Pia yeye na wenzake wawili wameanzisha kundi la muziki lililo chini ya producer Lamar, Shostiz.
6. Linah
IMG_7744-600x400
Nani asiyemfahamu Linah? Ni miongoni mwa wasanii wa kike wenye sauti tamu kuwahi kutokea Tanzania. Pamoja na Mungu kumpa sauti, amempa pia urembo unaowadatisha wanaume wengi.
7. Baby J
baby ja
Baby Jay ni msanii kutoka Zanzibar ambaye mara nyingi amekuwa karibu na kundi la Offside Trick. Macho yake huwachanganya wanaume wengi.


8. Shaa
397451_10150513227183570_380570125_n
Sarah Kaisi aka Shaa ni mrembo mwenye historia ya kufanya hits tu. Tangu ashiriki shindano la kusaka vipaji la East Africa Coca Cola Pop stars, hajawahi kusimama kwa kuachia ngoma kama Shoga, Siri ya Penzi na sasa akiwa na hit mpya, Promise.
9. Shilole
shilole
Shilole anafahamika kama malkia wa mduara kwa sasa na amekuwa kivutio kikubwa kwenye jukwaa kila anapotumbuiza kwa jinsia anavyojua kucheza na kiuno chake. Ameshatoa hits kibao zikiwemo Lawama, Viuno Tucheze na Dudu.
10. Vanessa Mdee
vanessa-mdee-m
Vanessa Mdee ni mrembo mwingine aliyeweka historia mwaka huu kwa kutoa single iliyoingia kwenye top ten ya nyimbo zilizopakuliwa zaidi (downloaded) mtandaoni, Closer. Pamoja na kuupata umaarufu kutokana na kazi yake ya utangazaji, mwaka huu amejipatia sifa kede kede kwa kuonyesha uwezo mkubwa katika kuimba.
11. Recho
543232_301717796563989_100001773129712_712957_1234630425_n
Recho ni msanii wa THT ambaye kabla ya kugundua kuwa ana uwezo mkubwa kuimba alijiona kuwa ni muigizaji wa filamu zaidi. Mpaka sasa ana nyimbo tatu tu, Upepo, Kizunguzungu na Nashukuru Umerudi lakini kila shabiki wa muziki wa Bongo analijua jina lake.