Huu Ndio Ukweli Kuhusu Kuvunjika kwa Kundi la Camp Mula
CAMP MULLA
Ni wiki kadhaa sasa toka kuripotiwa kwa mara ya kwanza habari za
kutengana kwa kundi la muziki kutoka nchini Kenya ambalo linafahamika
kwa jina la 'Camp Mulla' huku
mashabiki wake wakibaki njia panda wasijue nini kinaendelea ndani ya
kundi hilo lililojizolea umaarufu duniani koke. Hata hivyo tayari
wasanii wanaounda kundi hilo wamefunguka na kuweka wazi
ukweli wa jambo hilo ili kuwatoa hofu mashabiki wao lukuki.
Wasanii hao wa miondoko ya Hip Hop wameelezea kuwa kutengana kwao
haimaanishi ndio mwisho wao katika kufanya muziki, bali kila mmoja
ameona ni bora ajishughulishe na project zake binafsi. Imeelezwa kuwa 'Taio Tripper, K'cous na Miss Karun' wanatarajia
kuondoka nchini kwa ajili ya kujiendeleza zaidi na masomo wakati
'Shappaman' ataendelea kuwepo nchini Kenya na kuendelea kufanya shughuli zake za kimuziki From: kizobrax