Blogger Widgets

May 28, 2013

Fuatilia Hiki Kisa Kilichotokea Cha Dr.Cheni Kulishwa Sumu Kwenye Sherehe Mpaka Kukimbizwa Hospitali

Dr. Cheni alishwa sumu, Lulu achanganyikiwa, Soma stori nzima ilivyokuwa hapa.


Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.
Akiongea na bongo movies leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.
Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema.
Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo.
Pole sana Dr. Cheni.

No comments:

Post a Comment