Rapper kutoka kundi la weusi ,Joe Makini ametangaza kutokuachia ngoma yake aliyotarajia kuitoa siku ya tarehe 30, kupitia ukurasa wake wa facebook, Joe amesema amesogeza mbele kuachia ngoma hiyo ikiwa ni pamoja na show aliyokuwa anatarajia kuifanya ndani ya club 71 Tegeta
huku Mwana FA pia ameahirisha ile show iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu "the finest" iliyokuwa inatarajiwa kufanyika siku ya ijumaa hii, ili kuupisha msiba mkubwa uliotufika watanzania, msiba ambao kwa hakika wengi wameumia, msiba wa msanii wa hiphop Albert Mangwea a.k.a Ngwea, Kala pina pia ametangaza kuahirisha show yake iliyokuwa ifanyike siku hiyo hiyo,
tumepata
msiba mkubwa wa msanii mwenzetu ngwear kwa nawaomba radhi funz wote
kuwa tumeiharisha show yetu ya tarehe 31 msasani club mpaka
ntakapowatangazia mda huu 2naomboleza
huku Izzo B nae akitangaza kuahirisha pia kwa show yake iliyokuwa ifanyike mkoani kwake mbeya.
No comments:
Post a Comment