KIJANA
Ramadhan Suleiman Mussa ‘Rama mla watu’ na mama yake Khadija Ally, leo
wameachiwa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kubainika
kuwa mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo (mla watu) alifanya kosa la
mauaji akiwa na matitizo ya akili. Hata hivyo Rama Mla Watu,
ataendelea
kukaa katika hospitali ya wagonjwa wa akili ya Isanga mkoani Dodoma
mpaka akili yake itakapokuwa sawa ndipo ataachiwa kuwa huru mtaani ili
asije akawadhuru watu wengine. Khadija Ally yeye ameachiwa huru. Rama
alijizolea umaarufu mkubwa mwaka 2008 baada ya kukamatwa akiwa na kichwa
cha mtu kinachodaiwa kuwa ni cha mtoto Salome.
From:GPL
No comments:
Post a Comment