NANUKUU KUTOKA KWA DIAMOND Napenda kumshukuru Mungu kwa siku ya leo kuwa mahali hapa mzima kabisa wa afya..... Napenda kumshukuru mungu hata kwa wale ambao awakuiona siku ya leo na n.k Kwa mara Nyingine tena Nawaletea tena Mpambano kati ya Diamond Platnumz & Nay wa Mitego.....Yani Bongo Fleva VS Hip Hop......Baada ya Tukio zima la hatari lililotokea pale mbagala Darlive kwa kila mmoja kushambulia vibaya Jukwaa na kuweka historia,wananchi wakawa wanahitaji kujua Mshindi ni nan....? Asa katika kudhihirisha Ubora wa Bongo Fleva & Hip Hop Tumeamua kumalizia Ubishi wetu kwa Pamoja tena wananchi na wakazi wa Dar Es Salaam waje wenyewe kutoa maksi na maoni kusudi tumpate mshindi...... Kati ya sisi Kwenye show viuno mbele Mbele au Hip Hop watoboa Pua....!!
Kutokana na Mpambano kuwa mkali Darlive na Kutambulisha Video ya Muziki Gani,Tukashindwa pata Mshindi ndo Mahana Video aikuweza kuwekwa Kwenye Mtandao kama Ilivyotarajiwa....!!
Kwa Mara ya kwanza Tena Ndani ya Ukumbi wako wa Kijanja..... Pale Masaki,New Maisha Club Mataa yanapowakaga wakaga.......Pembeni I Myself Diamond Platnumz & Kulia ntakuwa na My Brother Nay wa Mitego..... Tutaenda kukiwasha tena kwa moto zaidi ya Darlive....Safari hii lazima mshindi apatikane iwe isiwe...!! Iwe kwa Njia ya kura zenu tujue kabisa Muziki upi unatamba mbele yenu....!!
Hii ni Yenu kwa Umoja tena Usikose kufika kumaliza utata ....Kwa Kiingilio cha Tsh 10,000/= ya kitanzania Siku ya Tarehe 26.5.2013 kuanzia saa 3 usiku mpaka Majogoo...... Tutaakikisha ile maisha club yote lazima steji zivunjike Mahana Historia mpya inaenda kuandikwa pale.... Ballerz n Divaz Hii inawahusu sana....Siku Hiyo kama wewe ni mtoto wa Town utakuwepo hapa Kuona Nini kitatokea.....Baada ya Hapo tutawashukuru Mashabiki zetu kwa Video ya Mwaka,Kichupa Bora kwa mara ya kwanza ndani ya maisha club utakuwa wa kwanza kuiona utakaefika hapo na Suprise Kibao........
|
No comments:
Post a Comment