Baada ya ajali hiyo Chris alipaki gari yake mbele ya gari aliyoigonga aina ya Mercedes Benz na kusimama pembeni huku dada mwingine wa kizungu (ambaye gari yake imegongwa) akiwa busy na simu. Wakati huo Karrueche Tran alikuwa busy na simu yake ya mkononi akijaribu kufanya u-paparazzi kwa kupiga picha gari waliyoigonga.
Mapema mwezi huu Karrueche alihudhuria moja ya birthday parties za Chris Brown, na Chris hakusita kumpa birthday wishes Karrueche kupitia twitter siku chache zilizopita kitu ambacho kiliashiria bado wana ukaribu.
Tukio hili limefungua upya uvumi kuwa huenda Chris Brown na Karrueche Tran wamerudiana japo bado hawajatamka rasmi ikiwa ni siku chache toka Chris aachane na Rihanna.
From:Bongo5
No comments:
Post a Comment