Muda
mfupi uliopita spika wa bunge, Anna Makinda amelazimika kusitisha
shughuli za bunge mwanzoni tu mwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani
iliyokuwa ikisomwa na waziri kivuli wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni
na Michezo, Joseph Mbilinyi aka Sugu.Kauli kwenye hotuba hiyo
iliyobabisha
spika wa bunge asitishe shughuli za leo hadi jioni ilisema, “Tanzania
imegeuka chini ya usimamizi wa wizara ya serikali hii ya CCM kuwa taifa
linalotoka nyara wanahabari, kuwatesa, kuwangoa kucha na meno, kuwatoboa
macho, kuwamwagia tindikali na hata kuwaua.”
Spika amesitisha bunge hilo ili kupata muda wa kuipitia hotuba hiyo kuondoa kauli za uchochezi.
Sikiliza Alichokisema Hapa Chini
Sikiliza Alichokisema Hapa Chini
No comments:
Post a Comment