Blogger Widgets

May 27, 2013

Vituko:Check Huyu Mwijiristi Aliyekula Kichapo Cha Hatari Baada ya Kutoa Mahubiri Kwenye Basi Baada ya Kuangusha CONDOM katikati ya Biblia


HALI tete na ya taharuki imezuka katika jiji la LAGOSI huko Nchini Nigeria mara baada ya Mwinjilisti mmoja aliyejulikana kwa jina la Mr John Mbakogwu.

Mr John Mbakogwu aliushangaza umati mkubwa ambao walikuwa ndani ya basi hilo wakisafiri kulekea maeneo mbali mbnali na kuacha taswira ambbayo haikuweza kueleweka kwa haraka kutokana na Mr John Mbakogwu kuonekana akihubiri kwa hisia kali huku akiwasisitiza wanajamii kuacha Dhambi kwa siku za mwisho zimefika,
  
Wakati akiendelea kutoa neno la Mungu Ghafla Condom ambayo alikuwa ameihifadhi ndani ya kitabu kitakatifu cha BIBLIA ndipo ilipoanguka chini huku abiria waliokuwa wakionekana wakiguswa na mahubiri ya mhubiri huyo wakishuhudia kwa macho yao na kubaki wakishanga kwa kutoamini lililotokea. Ndipo waumini hao waliposhikwa na hasira na kuanza kumshambulia kwa kumchapa makonde ya Nguvu na mwishowe raia wema ndipo walipoamua kumgombelezea kutoka kwenye Umati huo wa waumini wenye hasira na hivyo kufanikiwa kusalimisha uhai wake huo ambao ulionekana kuwa rehani

No comments:

Post a Comment