Tukio
hilo lililowashangaza wengi lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita
katika gesti moja iliyopo Sinza jijini Dar. Awali Flaviana na bwana wake
huyo walichukua chumba baada ya kushindwa kurudi nyumbani kutokana na
kuzidiwa na kilevi.
Ilikuwaje fumanizi likatokea?
Ilielezwa kuwa wakati wawili hao wakiingia kwenye chumba cha gesti
hiyo, Flaviana alikuwa bwii hivyo ‘kuzima’ kwenye kochi na kushindwa
kufanya chochote.
“Wakati Aron akiwa chumbani pale, alifika shosti wa Flaviana aitwaye
Dina na kwa kuwa Flaviana alikuwa hajitambui, wawili hao walianza
kupeana malavidavi.
“Flaviana akiwa amelala alikuwa kama vile anasikia watu
wakishughulika lakini alishindwa kufanya chochote kutokana na kuzidiwa
na pombe.
“Wale wakaendelea kubanjuka. Ilipofika saa 12 asubuhi Flaviana
akapata nguvu na kuamka kwenda kujisaidia, aliporudi akabaini shosti
wake amemsaliti na ndipo alipoanzisha timbwili,” alidai mtoa habari wetu.
Flaviana apigia simu mapaparazi
Wakati timbwili hilo likiendelea chumbani hapo, Flaviana alipata
mwanya wa kuwapigia simu mapaparazi ambapo ndani ya muda mfupi walifika
na kumshuhudia Dina akiwa ndani ya Bajaj huku akivaa nguo kabla ya
kumuamuru dereva kuondoka kwa spidi.
Naye mwanaume ambaye alikuwa ndani ya chumba cha gesti hiyo,
aliposikia waandishi wamefika, alitokea mlango wa nyuma akiwa amevaa
‘boksa’ na tisheti, akaacha suruali yake chumbani hapo.
Akizungumza na Risasi Jumamosi huku akiwaonesha mapaparazi kitanda
kilichokuwa vululuvululu, kilichotumika katika usaliti huo pamoja
kondom, Flaviana alisema: “Nimeumia sana, yaani nimesalitiwa nikiwa
humuhumu chumbani, Aron kanidhalilisha sana na huyo Dina naye kumbe siyo
mtu, nitahakikisha namsaka nimshikishe adabu.”
No comments:
Post a Comment