Blogger Widgets

June 22, 2013

Makubaliano ya Diamond Platnum na M2 THE P

Msanii wa bongo fleva mwenye mafanikio makubwa zaidi Tanzania Diamond Platnumz, jana (June 19) amekutana na aliyekuwa rafiki wa karibu wa marehemu Albert Mangwea anayefahamika kama M 2 The P, na inavyoonekana wana mpango wa kufanya kitu pamoja.
Diamond na M2 The P1
Platnumz ameweka picha katika website yake akiwa na M 2 The P ambaye sasa anaonekana mwenye furaha inayoashiria kuimarika zaidi kwa afya yake.
Katika picha hizo Diamond aliandika,
“Siku ya jana katika mishe mishe zangu nilikutana
na ndugu yetu na mwanmuziki mwenzetu,M 2 the P ambae
alikuwa ni mtu wa kalibu na


marehemu Ngwair…kukutana kwetu tulipata fursa ya
kuzungumza mengi nna Mungu akipenda..maybe we gonn do
something”

Diamond-3
Hit maker huyo wa ‘Kesho’ yuko katika maandalizi ya mwisho ya safari yake ya Comoro anayotegemea kwenda kufanya show hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment