Blogger Widgets

June 29, 2013

Picha zikionesha Jinsi Huyu Binti alivyovua Nguo na Kuanza Kutoa Zawadi Huku akiwa makalio Yake Nje


Ni aibu iliyoje! Mrembo mmoja, mkazi wa Kigogo, Dar es Salaam, aliyedaiwa kuwa ni mchumba wa mtu ambaye jina lake halikupatikana, alikatikiwa mshipa wa aibu na kuvua nguo katikati ya sherehe ya ‘birthday’ ya mtoto.

Kwa mujibu wa MPEKUZI wetu , tukio hilo lililojaa laana lilijiri ndani ya Ukumbi wa Palm Tree Kigogo, Dar, Juni 19, mwaka huu ambapo kulikuwa na sherehe ya kuzaliwa mtoto aliyetajwa kwa jina moja la Junior aliyekuwa akitimiza miaka 5.

Chanzo hicho kilieleza kwamba, mnyange huyo ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa, alitimba ukumbini hapo akiambatana na mwanamume aliyedaiwa ni mchumba’ake.
Kilidai kwamba, mara baada ya kujitwalia moja ya meza ukumbini hapo, wawili hao walianza kugida ulabu kwa staili ya ‘tuone nani mkali wa kumeza maji’.
MPEKUZI wetu alidadavua kwamba, haukupita muda mrefu, mwanamume aliyeambatana na mrembo alionekana akizungumza na simu ambapo alimwacha mwanadada huyo na kutoka nje.

Ilidaiwa kuwa, kitendo hicho kilimpa nafasi mrembo huyo ambaye alianza kufanya madudu mbele ya kadamnasi bila kujali idadi kubwa ya watoto waliokuwa ukumbini.


AANZA KUPANDISHA KIGAUNI

Chanzo chetu kilidai kuwa, inaelekea jamaa aliyekuwa na mrembo huyo alipata ‘dharura’  hivyo hakurejea.
Ilisemekana kwamba, muda wa kutoa zawadi ulipowadia, mchumba huyo wa mtu alichafua hali ya hewa baada ya kuanza kupandisha kigauni kifupi alichokuwa ametinga na kuacha nusu ya mwili wake sehemu yote ya chini ikiwa wazi.



 AMALIZIA HADI ‘KUFULI LAKE ’

Chanzo kiliweka wazi kwamba, mrembo huyo alimazia kuvua nguo nyingine hadi ‘kufuli’ na kubaki mtupu kama alivyozaliwa hivyo kuwafanya watoto kushuhudia sinema ya bure.




  ATOA ZAWADI ZAKE KWA MAKALIO AKIWA UCHI WA MNYAMA

Iliendelea kudaiwa kuwa, mrembo huyo aliharibu kila kitu pale alipochomeka noti ya buku 10 kwenye nyeti zake na kwenda kumtunza mama wa mtoto.
“Kama hiyo haitoshi, yule binti aliweka sharti kuwa hakuna kupeleka ‘hela’ kwa mama mtoto na badala yake watu wamuwekee kwenye makalio.

“Wapo waliokubali ‘then’ akaenda na kumlazimisha mama mtoto azichukue,” kilisema chanzo hicho.



Chanzo kiliendelea kuweka kweupe kwamba, mara baada ya kuona tukio hilo, baadhi ya wazazi waliokuwa na watoto wao ukumbini hapo walimaindi hivyo kuondoka kwa aibu.


No comments:

Post a Comment