The Prezidaa CMB Prezzo ambae alikuwa mshiriki wa shindano
la Big Brother Africa msimu uliopita amejiunga na project ya watu wanaompigia
debe the boss Lady toka Kenya Huddah Monroe ambae alikuwa mpenzi wake ili asitoke
kwenye jumba hilo wiki hii.
Prezzo ameitumia akaunti yake ya twitter kujiunga na kile
kinachofahamika kama #ProjectSaveHuddahMonroe na yeye ameandika tweet
inayosomeka, “ SMS the Word VOTE HUDDAH to 22626 #ProjectSaveHuddahMonroe.”
Akatupia tweet nyingine kuwahamasisha zaidi wakenya wawe na
khari zaidi, “That’s the spirit 254#LetsGo!RT@MilGoddie:
Its HUDDAH or Nothing @AMB Prezzo_”
Inawezekana pia Prezzo akawa anarudisha fadhira kwa X girlfriend
wake huyo kwa kuwa alimsaidia pia wakati akiwa katika jumba hilo kuongeza kura za
kumuweka katika nafasi nzuri zaidi.
Huddah, Selly, Denzel, Betty na Natasha wako katika hatari ya
kuondoka katika jumba hilo wiki hii, kura za watazamaji ndizo zitakazomuokoa mshiriki
ama zisipotosha anaondoka.
No comments:
Post a Comment