Member wa kundi la Chemba Squared ambalo ni kundi lililomjumuisha marehemu Albert Mangwea, Mez B wa Area C, na Noorah a.k.a baba Star amepaza sauti yake akiwa jijini Mwanza alipopewa nafasi ya kuzungumzia jinsi alivyopokea habari za kifo cha msanii mwenzake (Ngwea) na ameliweka hewani ombi lake kwa mheshimiwa rais Jakaya Kikwete.
Dark Masters amemuomba mheshimiwa rais aingilie kati na
awaangalie pia wanachemba wasife masikini, “tufikirie wana chemba tusife
masikini.”
Pia ameelezea jinsi alivyopokea taarifa za msiba za msanii
mwenzake kwa masikitiko, na katika hali ambayo hakuitegemea lakini anasema
mwisho ilimbidi aamini kwa kuwa hiyo ni njia yetu wote.
Mwili wa Marehemu albert Mangwea aliyefariki huko
Johannesburg Afrika kusini unatarajiwa kufika Tanzania jumapili hii saa nane
mchana.