Blogger Widgets

July 29, 2013

Fahamu Kilichosababisha Mshiriki Nando Kutoka Tanzania Kufukuzwa Ndani ya Jumba La Big Brother Africa


Jana usiku mara tu baada ya Sulu na Annabel kutolewa kwa kura za watazamaji, Big Brother aliwaita washiriki pamoja katika kikao cha dharura kufuatia ugomvi uliotokea kati ya Nando na Elikem.

Itakumbukwa kwamba siku ya ijumaa ilitokea hali ya kutoelewana kati ya Nando na Elikem. Wawili hawa walitukanana sana na kutishiana mno. Ugomvi huo ulianzishwa na Nando.

Kwa mujibu wa sheria za Big Brother mwaka huu, kuanzisha ugomvi ni kosa ambalo hupelekea kupata 'strike' ama onyo.

3 strike rule ni mtindo unaotumika msimu huu. Kwa mujibu wa Big brother, yeyote atakaye fanya makosa matatu makubwa na kupewa maonyo matatu basi moja kwa moja anatakiwa atimuliwe..

Sheria hiyo imetumika kumtimua Nando kwa sababu 1. Alianzisha ugomvi siku ya Ijumaa, 2. Alishiriki ugomvi na Elikem na 3. Alitishia maisha, "I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die"...

Katika kipindi cha wiki 9 za ushiriki wake katika jumba hilo, Nando amekutwa na misuko suko kadhaa ikiwemo kuwahi kukutwa na kisu katika Party ya Channel O pia kukutwa na mkasi chini ya kitanda kitu ambacho ni kinyume cha sheria za big brother.

Kutokana na ugomvi huo Elikem alipata strike moja.

Big brother alimtaka Nando aondoke katika jumba lake hilo na kutumia fursa hiyo kuwataka washiriki wengine waishi kama watu wazima.
 
From Big Brother Africa Website
Tanzania's Nando has been disqualified from the Big Brother House.

After tonight's Evictions that saw Annabel and Sulu being given the boot, Big Brother then gathered all of the Housemates in the living room.

Today Big Brother reproached Nando for the fight that he had with Elikem on Friday. The heated face-off with Elikem saw the two fellas exchanging fiery words between them. Nando is the one that instigated the fight. Instigation and provocation is a violation of the Big Brother rules.

For this fight Nando received his second Strike and Elikem was has served with his first Strike. Afterwards the Tanzanian was called into the Diary Room. He was given his third Strike for making threats against Elikem's life, saying: "I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die".

And he was also caught sleeping with scissors under his bed and this is not the first time that he has been caught with a weapon in the House. The troubled young fellow has had a dramatic nine weeks in The Chase. Last month he was served with a a Strike and a stern warning from Big Brother after he was found carrying a knife to the Channel O Party. The possession of weapons or intention to be violent in the House another violation of the Big Brother rules.

After the Diary session Nando was told to immediately exit the House. Big Brother then gave a warning to the Housemates to conduct themselves as adults.

No comments:

Post a Comment