Blogger Widgets

July 8, 2013

Story Ilivyokuwa Mpaka Wema Sepetu akamnasa Vibao Manager wa Hotel

Wema Sepetu.
Mwaija Salum na Denis Mtima
DIVA wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo (jina tunalo) iliyopo Kawe Beach, jijini Dar.

MAELEZO YA MENEJA
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.

WEMA, WENZAKE WAZIDIWA NA KILEVI
Meneja huyo akaendelea kusema, ilipofika  saa tano usiku, Wema na marafiki zake  walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo.
Aliongeza kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake, aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa makusudi huku meneja huyo akishuhudia.
Meneja akasema: Wakati wanaondoka, nilimfuata yule jamaa mpaka nje, nikamuuliza ni kwa nini amevunja glasi kwa makusudi, akanijibu kwa dharau huku akinitukana na kutishia kunipiga, akawa ananiuliza hiyo glasi ni shilingi ngapi kwani?
WEMA AANZA KAZI YA KUSHUSHA KIPIGO
Aliongeza kuwa swali lake kwa kijana huyo lilionesha kumkera sana Wema, kwani alitoka kwenye gari na kuanza kumlamba vibao visivyo na idadi meneja huyo huku akimpa maelekezo kwamba akashitaki popote na hawezi kufanywa kitu kwani yeye ana nguvu kwenye nchi hii.
“Niliamua kupiga simu Kituo cha Polisi Kawe, wakaja kuangalia mazingira kisha nikaondoka nao kwenda kufungua kesi kituoni.”
Faili la kesi hiyo linasomeka KW/RB5988/2013, SHAMBULIO. Hadi tunakwenda mitamboni, Wema anasakwa na polisi ili apandishwe mahakamani.
TUJIKUMBUSHE
Mwaka 2009, Wema alidakwa na Polisi Kituo cha Magomeni na baadaye kupandishwa katika Mahakama ya Kinondoni, Dar kwa Hakimu Emilius Mchalu kwa kosa la kuvunja kioo cha gari la aliyekuwa staa wa filamu Bongo, Marehemu Steven Kanumba chenye thamani ya shilingi milioni moja.
Hata hivyo, Kanumba aliamua kuifuta kesi hiyo kwa sababu ya kutaka amani. Wakati huo Wema alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mjasiriamali aitwaye Jumbe Yusuf Jumbe.
ALIMTISHIA MAISHA BOB JUNIOR
Kama vile haitoshi, mwaka 2011, Wema huyohuyo alilikwaa soo jipya, akakamatwa na Polisi wa Oysterbay na kufikishwa Mahakama ya Mwanzo, Kinondoni kwa kosa la kumtusi na kumtishia maisha mwanamuziki wa Bongo Fleva, Rahem Nanji ‘Bob Junior’.
Katika kesi hiyo, Hakimu Mariam Masamalo alimtia hatiani Wema na kumhukumu  kwenda jela miezi sita au faini ya shilingi elfu arobaini ambapo alilipa feha hizo. Wakati huo, Wema alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamon

No comments:

Post a Comment