Mwigizaji anayetarajia kujifungua hivi karibuni, Flora Mvungi
amesema kuwa wamekubaliana na Mume wake H-baba kumpa jina la Tanzanite
mtoto wao huyo anayetarajia kujingua hivi karibuni.
Flora alisema mumewe alichagua jina hilo kwa sababu mtoto wao huyo
anatarajiwa kufahamika kimataifa kutokana na umaarufu atakaokuwa nao na
ikizingatiwa kuwa madini ya Tanzanite yanapatikana Tanzania pekee.
Akinukuliwa na GPL flora alisema “Kama nikijifungua salama awe
mtoto wa kiume au wa kike ataitwa jina hilo na atakuwa tofauti sana na
msanii wa muziki anayejiita Tanzanite kwa kuwa yule hilo siyo jina lake
halisi bali ni a.k.a tu,” alisema Flora.
Flora na H: Baba walifunga ndoa hivi karibuni na wakati wowote wanatarajiwa kupata tunda lao la kwanza kwani Flora ni mjamzito.
No comments:
Post a Comment