Kufuatia rapa A$ap
Rocky kuonekana katika pozi za utata na Rihanna hivi karibuni na kufikia
hatua ya watu kuanza kufikiri kuwa huenda kuna kitu kimeanza kati yao,
Rapa huyu ameamua kufafanua kilichokuwa kinatokea eneo la tukio.
A$ap Rocky amesema
kuwa hataki kujiingiza katika matatizo ya tetesi kumhusu yeye na Rihanna
kwasababu hakuna kitu chochote kinachoendelea kati yao, na yeye na
Rihanna ni marafiki wakubwa tu.
Rapa huyu amesema
kuwa anampenda Rihanna kwasababu anasapoti kazi zake na hakuna cha
ziada, ingawa taarifa za chini chini zinaweka wazi kuwa, Tokea wawili
hapa walipofanya tour pamoja, wamejijengea ukaribu wa ajabu ambao unazua
maswali mbalimbali kila mara wanapokuwa pamoja.
No comments:
Post a Comment