Blogger Widgets

August 3, 2013

Picha za Fumazi la Ajabu la Bi Khadija Ndani ya Mwezi Huu Mtukufu Baada ya Kufumaniwa na Mumewe




TIMBWILI zito limeibuka baada ya mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Samora kumnasa ‘live’ mkewe Hadija akimsaliti kwa kuvunja amri ya 7 (usizini) na hawara ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, tena kwenye chumba chao, Ijumaa lina ishu kamili.

 
Mshangao: mtuhumiwa akikodoa macho baada ya kunaswa live na mke wa mtu chumbani kwa mwenye mali.
Habari kutoka chanzo cha uhakika kilitonya kuwa Samora na Hadija ni wanandoa waliooana Bomani pale Magomeni, Dar, mwaka 2009 na katika ndoa yao wamebahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Tukio hilo la fumanizi lilijiri maeneo ya Kinondoni-Kwamsisiri, Dar nyumbani kwa wanandoa hao, majira ya saa 1:00 usiku, Julai 29, mwaka huu.
 
Aibu: mtuhumiwa akijaribu kuficha sura yake baada ya fumanizi hilo.
NDOA YATUMBUKIA NYONGO
Habari zilieleza kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, ndoa ya wawili hao ilitumbukia nyongo na kuingia kwenye mgogoro ambapo pamoja na kuweka mambo sawa, waliendelea kukwaruzana mara kwa mara.
 
Mshangao: Nisameheni jamani!
CHANZO NI NINI?
Ilidaiwa kuwa chanzo cha wawili hao kuhitilafiana ni kutokana na mwanaume kumtuhumu mkewe kutoa tunda nje ya ndoa.
Ikasemekana kuwa baadaye wapambe walimfuata Samora na kumtonya kuwa mkewe amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na kidume mwingine nje ya ndoa yao ndiyo maana amekuwa akimletea nyodo ‘mapichapicha’.
Iliendelea kudaiwa kuwa baada ya ndoa kutibuka, Samora alikuwa mnyonge na mwenye msongo wa mawazo hivyo ikabidi aikimbie nyumba kwa muda na kwenda kwa wazazi wake.
Ilisemekana kuwa, Samora alirejea nyumbani huku akifanya uchunguzi wa nguvu akiwatumia majirani kumpatia taarifa kuhusu kila mwanaume aliyeingia na kutoka nyumbani kwake yeye akiwa hayupo.
 
Bwana Samora akiwa na mkewe Hadija siku ya harusi yao.
KUMBE NI RWEKAZA
Uchunguzi wa Samora ulibaini kuwa, Hadija alikuwa ‘akibanjuka’ nje ya ndoa na mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Rwekaza ambaye ni mfanyakazi serikalini.
Habari za kina zilisema kuwa, Samora alitonywa kwamba jamaa alikuwa akitimba na gari aina ya Suzuki Swift 1.3 na siku nyingine alikuwa akilala hadi asubuhi bila tone la soni kuwa Hadija ni mke wa mtu.
 
Samora na Hadija wakiwa na wapambe wao siku ya harusi.
SAMORA AJIPANGA
Baada ya kupata uhakika huo ndipo Samora akajipanga kwa kuwatafuta vijana wa mtaani ili Rwekaza atakapofika nyumbani hapo kulala na mkewe wamvamie na kumfanyizia.
 
Mshikemshike: Samora (wa tatu kushoto) na wapambe wake wakitaka kumshushia kichapo mtuhumiwa.
RWEKAZA MTEGONI
Bila kufahamu kuwa anasubiriwa kwa hamu majira yaa saa 1:00 usiku, Rwekaza huyooo, akatinga nyumbani hapo na moja kwa moja akafikia chumbani kama kawaida yake.
Wakiwa chumbani, ilidaiwa kuwa waliendelea na mambo yao huku Rwekaza akiwa tumbo wazi na suruali yake amefungua zipu huku Hadija akiwa amesaula na kubaki na ‘kufuli’, kisha akajifunga khanga moja.
 
Hasira: Samora (kushoto) akimkunja mwizi wake baada ya kumfumania.
FUMANIZI KABANG’
Katika fumanizi hilo, Samora alitinga chumbani humo akiwa ameambatana na kundi la vijana kibao ambao walikuwa na lengo moja tu, kumfanyia kitu mbaya Rwekaza.
Wakiwa chumbani, kuliibuka bonge la timbwili baada ya Samora kumshuhudia mwenza wake aliyekula kiapo cha kutotengana naye akisaliti ‘laivu’ penzi lao.
Baada ya kuona machafuko makubwa ya hali ya hewa chumbani, mwanahabari wetu aliwataarifa polisi katika Kituo cha Kwamsisiri ambao walifika maeneo hayo na kufanya kazi kubwa na nzuri ya kuepusha balaa au mauaji kwa kuwa Samora alikuwa na hasira kali.
 
Albamu ikionyesha picha walizopiga Samora na mkewe Hadija wakati wakisaini kitabu cha ndoa.
KWELI NI MKE WA NDOA?
Ili kuthibitisha kuwa ni mkewe wa ndoa, Samora alizama kabatini na kuchomoa cheti cha ndoa na picha walizopiga siku ya ndoa yao zikiwaonesha wakiwa na tabasamu la ‘mimi na wewe milele’ kabla ya shetani ‘kufanya yake’ kwenye unganiko lao.
 
Wananchi wakiwa nje ya nyumba alipofumaniwa bwana Rwekaza.
MAJIRANI
Kwa mujibu wa majirani, tukio hilo liliwasikitisha wengi huku wakiamini kabisa kuwa ni nadra matukio ya mafumanizi kutokea katika kipindi cha mfungo.
“Jamani hata Mwezi Mtukufu? Ni aibu sana kwa mke kuingiza mwanaume mwingine kwenye chumba cha mumewe. Kweli hili fumanizi ni kiboko,” alisikika mmoja wa majirani hao walioshuhudia tukio hilo muda mfupi baada ya kufuturu.
 
Gari la mtuhumiwa aina ya Suzuki Swift 1.3 likiwa nje ya nyumba alipofumaniwa.
SAKATA LINAENDELEA
Hadi gazeti hili linaondoka eneo la tukio wahusika wote walikuwa kituoni hapo hivyo tunaendelea kulifuatilia sakata hilo kwa karibu sana na pia kuwapata wahusika wazungumzie kilichojiri.

No comments:

Post a Comment