Check Picha za Mfanyabiashara Maarufu Alivyotupiwa Jeneza Lenye Maiti Ndani Yake Kwenye Malngo wa nMlango Wake
JENEZA lenye mwili wa mtoto mchanga, limezua taharuki kwa wananchi na
wakazi wa Mtaa wa Ihago, Kata ya Mahina, Wilaya ya Nyamagana jijini
Mwanza.
Tukio hilo la kushangaza na la aina yake, lilitokea Agosti
29, mwaka huu, majira ya saa 12:00 asubuhi baada ya kugunduliwa na
mfanyabiashara Ester Musa (28) likiwa limetelekezwa kwenye mlango wa
mgahawa wake.
Jeneza hilo linaaminika kufukuliwa na watu wasiofahamika kwenye moja ya makaburi eneo la Mahina jijini hapa.
Akizungumza
na gazeti hili kuhusiana na tukio hilo, Ester anayemiliki na kuendesha
mgahawa alisema, alifika katika eneo lake hilo la biashara, ghafla
akapigwa na mshangao baada ya kuona jeneza likiwa mbele ya mlango wa
mgahawa wake.
“Nashindwa kujua nini maana ya tukio hili sababu hivi
karibuni nilikuta barua imebandikwa ukutani ikinitaka nihame kutoka
eneo hili, vinginevyo nitaona nitakachofanyiwa. Leo nimekuta jeneza
mlangoni,” alisema Ester na kuongeza;
“Tukio hili nalihusisha na
imani za kishirikina lakini kubwa linachangiwa na wivu wa
kibiashara.Tangu lizaliwe sijawahi kuona jambo kama hili. Hapa sijawahi
kugombana na mtu yeyote nashangaa kufanyiwa kitendo cha namna hii katika
eneo la biashara yangu.”
Mwenyekiti wa mtaa huo, Anthony Deus
alisema kitendo cha kufukua mwili wa marehemu tena mtoto mchanga, si cha
kibinadamu na ni tukio la kusikitisha katika jamii, hivyo
watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
Kaimu Kamanda wa
Polisi, Mkoa wa Mwanza, ACP Christopher Fuime, alikiri kuwapo kwa tukio
hilo na kusema hakuna mtu aliyekamatwa akihusishwa nalo.
“Tunaendelea
na uchunguzi lakini hadi sasa hakuna aliyekamatwa akihusishwa na tukio
hili la kusikitisha… wananchi wameuzika upya mwili wa mtoto huyo,”
alisema.
No comments:
Post a Comment