Blogger Widgets

September 22, 2013

Hiki Ndio Kilio cha Penny Kwa Diamond Platnum


Penny au sukari ya Diamond




Yule mwanadada anayewapandisha presha wadada wa mujini Penny mungilwa ama ukipenda muite sukari ya Diamond amechonga nakueleza mengi kuhusu sukari wake huyo ambaye kwa sasa yupo nchini malaysia katika bonge la show.



Penny ambaye pia ni mtangazaji wa Tv hapa nchini tanzania amesema kwake hakuna wakati mgumu anaoupata kama Diamond akisafiri penny aliielezea kuwa anaumia sana kumkosa sukari wake huyo na mara nyingi hujikuta akiugua kabisa kama diamond akimtajia safari.


Penny ameyasema hayo wakati diamond akiwa nchini malaysia kikazi alikokwenda kupiga bonge la show nchini humo na kumuacha penny ndani ya bongo....Kiukweli hakuna wakati mgumu na huwa naumwa kama diamond akisafiri yaani huwez  amini nimemzoea sana bby wangu jamani alisema penny
Muandishi wetu alimdadisi kutaka kujua kwanini aumwe au hamtakii mwenzie mafanikio maana mtu kama diamond anaposafiri kikazi ujue ndio anaingiza mkwanja na pia anajitangaza yeye na nchi yetu kiujumla ambapo panny alianza kwa kuna kuwa hamtakii mafanikio nakuongeza kuwa..No nafurahi d anaposafiri na ninamtakia mafanikio mema ila nataka ujue hii nikutokana na jinsi tulivyoshibana na kuzoeana na sio mimi pekee yangu hata yeye nikisafiri hapati usingizi kucha ni simu hadi kunakucha alisema mwanadada huyo


Penny mapozi

Hapo ni kama alimchokoza mwandishi wetu nakujikuta akitaka kujua kama huwa kuna wakati wanasafiri wote au lah!!,,Mbona mara nyingi tu alijibu kifupi na ndipo nilipomuuliza kwanini hali hiyo inamtokea akasema.... Unajua mimi na Nassebu tumekuwa kama mapacha sasa mmoja akienda mbali na mwenzie basi aliyebaki huwa kama mgonjwa na ndio maana diamond akiwa mbali na mimi utakuta tunaongea na simu hadi mimi na mzuia maana hatulali sasa na hii ni ili kunifanya nione tupo wote kiukweli tumezoeana sana aliendelea kusema penny 
Hilo bango hapo juu ndio kazi liyompeleka Diamond huko Malaysia ambapoa kwa mujibu wake ni kwamba atahakikisha anaacha jina huko kama kawaida yake.

No comments:

Post a Comment