Menina akifanya yake jukwaani.
Walter Chillambo akiimba
Mashabiki waliojitokeza wakishangilia
Fuse ODG akifundishwa kucheza kiduku na shabiki
Wasanii wa Marco Chali Foundation wakiwa katika picha ya pamoja.
*********************************************
MSANII
wa muziki wa kileo kutoka nchini Ghana Fuse ODG, Azonto amewapagawisha
mashabiki wake wa Bongo baada ya kuchanganya staili yake ya uchezaji
Azonto pamoja na ile ya Kiduku ambayo ni maarufu ya hapa nchini, wakati
wa shoo yake iliyofanyika kwenye viwanja vya Chuo cha Ustawi, mwishoni
mwa wiki.
Fuse
ODG ambae anajulikana zaidi kama Azonto alipanda jukwanii majira ya saa
tisa kasoro usiku baada ya wasanii wengine wengi kumaliza kutoa
burudani. Ilikuwa ni baada ya
kupanda kwa kundi la Tip Top Connection huku likiongozwa na msanii Madee
pamoja na msanii Chid Benz ambae aliimba nao kama msanii rafiki.
Baada
ya kumalizika kwa shoo hiyo kwa wasanii hao wa hapa nyumbani ndipo
alipopanda msanii Azonto ambae alisikika akihamaisha kwa kutajan maneno
ya kiswahili kama vile, Nawapenda, Mambo vip na piga kelele.
Msanii
huyo kwa kiasi kikubwa alifanikiwa kuwaweka karibu zaidi wapenzi wake
wa burudani hasa pale alipowapandisha jukwaani vijana wawili kucheza nao
Azonto na Kiduku.
Alianza
kwa kuwachezesha Azonto na kisha muda huo huo aliwabadilishia muziki na
kucheza nao kiduku huku mwenyewe akiahidi kuiendeleza zaidi staili
hiyo.
Akizungumza
baada ya onesho hilo alisema kuwa amefurahishwa na namna ambavyo
wasanii na watu wa Dar es salaam walivyompokea na kuahidi kuwa
ataiendeleza staili ya kiduku nakuitangaza zaidi.
"Mimi
kwanza niliwahi kuja Tanzania na kufikia kule Arusha kwa mapumziko na
kwa sasa nimekuja kwa kazi na nipo tayari kufanya kazi na wasanii wa
Tanzania kwani mwisho wa siku sisi ni waafrika ambao tunatakiwa
kusaidiana na kuendelezana" alisema Azonto.
Wasanii
kama vile Madee, Tunda Man, Water Chilambo, Menina Atik, kundi la Navy
Kenzo, B Heats, Mabeste, Eskide, Mapacha na wengineo wengi pia walitoa
burudani safi siku hiyo
No comments:
Post a Comment