TASNIA
ya filamu Bongo imepata pigo lingine baada ya mwishoni mwa wiki
iliyopita kuondokewa na msanii aliyekuwa akichipukia kwa kasi
aliyefahamika kwa jina la Zuhura Maftah ‘Malisa’.
Malisa
alifariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar baada ya
kusumbuliwa na uvimbe kichwani kwa takriban miezi mitatu.
Wakizungumza
na gazeti hili mara baada ya kifo hicho, baadhi ya wasanii wa filamu
walielezea masikitiko yao na kusema hakika wamemkosa msanii ambaye siku
za baadaye angekuwa moto wa kuotea mbali.
“Kifo
chake kimetusikitisha sana, Malisa alikuwa mmoja wa wasanii ambao
walikuwa wakija kwa kasi, amefariki dunia wakati ndiyo kwanza nyota yake
ilikuwa imeanza kung’ara lakini kazi ya Mungu siku zote haina makosa,
akapumzike kwa amani,” alisema mmoja wasanii aliyeomba hifadhi ya jina
lake.
Msanii mwingine wa filamu ambaye huenda kifo hicho kimemgusa kuliko
wengine ni Yvonne Cheryl ‘Monalisa’ ambaye inadaiwa muda mfupi kabla ya
Malisa kufariki waliongea na kumwambia anaendelea vizuri.
Mmoja wa watu waliokuwa wakimhudumia Malisa hospitalini hapo
aliyefahamika kwa jina la Vanitha alisema: “Siku ya kifo chake
aliniambia nimpigie simu Mona aongee naye kwani hajamuona siku hiyo,
ilikuwa saa 12 jioni baada ya kumaliza kumuogesha.
“Waliongea
na kumwambia anaendelea vizuri. Baada ya Malisa kumaliza kuongea na
Mona niliondoka lakini nilipofika Surender Bridge nikapata taarifa kuwa
amefariki dunia,” alisema Vanitha.
No comments:
Post a Comment