Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameacha gumzo Jijini Mwanza alioweza kuongea na
wakazi wa jiji hilo pale alipoelezea jinsi gani wazazi wanapaswa kuishi
na watoto wao, Lulu ambaye kwa sasa yupo katika harakati ya kuhakikisha
kuwa kizazi kilicho chini ya miaka kumi na nane kinakuwa tayari
kukukabili changamoto za mihemko ya miili yao na yanayowakabili katika
makuzi yao.Akiwa jijini Mwanza aliweza kutoa somo kwa wazazi kuwa makini
na watoto wao kuhusu maisha ya kawaida na kuhakikisha wanawafuatilia
katika masuala ya masomo na mienendo yao katika maisha ya kawaida ili
kutambua kama kuna mabadiliko yoyote kutoka kwa watoto hao bila suala
hilo kuwaachia walimu na wasaidizi wa kazi.
Mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Benjamin Masanja kutoka Mwanza ambaye pia aliweza kumshuhudia Lulu amesema kuwa ni binti mwenye akili na uwezo mkubwa wa kujieleza na kwa mwendo huu anaamini kuwa anaweza kuokoa kizazi kikubwa chenye mitihani mingi katika makuzi yake yanayokabiliana na changamoto za utandawazi.
“Lulu ni dira njema kwa wale wote ambao wapo katika umri mdogo na wanakabiliana vishawishi vingi kutoka kwa wavulana na watu wazima kabisa, lakini pia kwa vijana wa kiume nao kujikuta wakiingia katika madawa ya kulevya hata ngono,”anasema Masanja.
Lulu ambaye ni balaozi wa tamasha la filamu linalojulikana kwa jina la Dar Filamu Festival , kwa sasa anatumia muda wake mwingi kuwashauri vijana ambao wapo katika mabadiliko ya utoto kuelekea ukubwani ili wasiweze kujiingiza katika matukio yanayoweza kuwasababishia matatizo.
Mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Benjamin Masanja kutoka Mwanza ambaye pia aliweza kumshuhudia Lulu amesema kuwa ni binti mwenye akili na uwezo mkubwa wa kujieleza na kwa mwendo huu anaamini kuwa anaweza kuokoa kizazi kikubwa chenye mitihani mingi katika makuzi yake yanayokabiliana na changamoto za utandawazi.
“Lulu ni dira njema kwa wale wote ambao wapo katika umri mdogo na wanakabiliana vishawishi vingi kutoka kwa wavulana na watu wazima kabisa, lakini pia kwa vijana wa kiume nao kujikuta wakiingia katika madawa ya kulevya hata ngono,”anasema Masanja.
Lulu ambaye ni balaozi wa tamasha la filamu linalojulikana kwa jina la Dar Filamu Festival , kwa sasa anatumia muda wake mwingi kuwashauri vijana ambao wapo katika mabadiliko ya utoto kuelekea ukubwani ili wasiweze kujiingiza katika matukio yanayoweza kuwasababishia matatizo.
No comments:
Post a Comment