Blogger Widgets

October 5, 2013

Habari ya Kusisimua Juu ya Huyu Mtoto aliyeongea akiwa na Miezi Miwili na Kutoa Ujumbe Mzito Huko Zanzibar

 MTOTO wa miezi 10, aliyetambuliwa kwa jina la Fahazal mkazi wa Kivunge amefikishwa mbele ya serikali ya mkoa wa kaskazini Unguja, baada ya mama yake mzazi kusema amekuwa akitokewa na maajabu na kwamba jamii iombe dua ili kunusuru kutokea vifo.
Mtoto huyo, ambaye anaishi katika kijiji cha Changani Kivunge wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja, ameonesha maajabu, baada ya kuanza kusema akiwa na umri wa miezi miwili, kwa kutaja majina ya Mwenyezi Mungu, Mtume Muhammad (SAW) na maneno ya kumtukuza Mwenyezi Mungu. 

http://3.bp.blogspot.com/_16Cq7BFJCfg/SwJQc6Db6-I/AAAAAAAABmc/wKlK0BUIyt4/s640/Capture.JPG Mkuu wa wilaya hiyo, Riziki Juma Simai, akizungumza na Zanzibar Leo, amethibitisha kuwepo mtoto huyo.
Alisema mtoto huyo amefikishwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa na familia yake baada ya mama yake aliyefahamika kwa jina moja la Dawa, kutakiwa kuwasilisha ujumbe alionao mtoto huyo kwa jamii.


Alisema kabla ya kuzaliwa, mama yake alisema kuwa alikutwa na mambo ya maajabu baada ya kujiwa na kiumbe akimueleza uwezo wa mtoto wake wakati akiwa tumboni na kumchagulia jina la kumpa baada ya kuzaliwa.
Mkuu wa wilaya huyo alisema, kiumbe hicho kilichokuwa katika mazingira yasioelezeka pia kilimtabiria mama huyo kwamba atazaa mtoto wa kiume.
Pia alimuambia baada ya mtoto huyo kuzaliwa atakuwa na mambo ya ajabu na kumtaka kumtunza na asimuogope na baadae kiumbe hicho kiliondoka.
Alisema baada ya tukio hilo, na siku zake za kuzaa kutimia alijifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Fahazal na ndipo alipoanza kushuhudua maajabu ikiwa ni pamoja na kuzungumza akiwa na miezi miwili.
Alisema mtoto huyo alikuwa akitamka maneno ya kumtukuza Mwenyezi Mungu ikiwemo Allwah, Yaraabi na kutaja jina la Mtume (SAW) huku akiwataja kwa majina watu waliokuwemo nyumbani kwao.


Mkuu wa wilaya hiyo alisema hivi sasa mtoto huyo, amekuwa akiwasomea dua watu wanaofikishwa kwake kwa matatizo ambapo huonesha ishara ya kuinua mikono juu ya kuitikia dua wakati ikisomwa.
Alisema kwa muda mrefu, familia yake iliendelea kuishi naye, lakini mama yake alifuatwa tena na kiumbe hicho na kumtaka kufikisha ujumbe wa mtoto huyo mbele ya jamii akitaka jamii iombe dua kwa wingi kwani vifo vingi vinaweza kutokea nchini.
Alisema kiumbe hcho kilirudi baada ya mama wa mtoto huyo kupuuza ujumbe wa mwanzo aliopewa na ndipo alipoamua kutafuta watu wa kumsaidia ambapo walimuelekeza kufuata viongozi wa dini.
Alisema, baada mama huyo kupokea ujumbe huo, aliamua kuutekeleza kwa kuwafuata baadhi ya walimu katika kijiji hicho kuelezea mkasa huo, ili aweze kupata msaada.
Viongozi wa dini walimtaka mama huyo, kulifikisha suala hilo katika ngazi ya serikali, kutokana uzito wake kwa jamii, ambapo walimshauri kuonana na uongozi wa mkoa.
Mkuu huyo wa wilaya alisema, jana asubuhi, alimpokea mama huyo akiwa na mtoto wake pamoja na shahidi ambaye ni mkaazi wa kijiji hicho ambapo walithibitisha maajabu ya mtoto huyo.
Alisema mtoto huyo huzungumza baadhi ya wakati na kwamba anazungumza lugha tofauti ikiwemo kiingereza, kiarabu.
Alisema wameifikisha familia hiyo kwa Mkuu wa Mkoa ili kufanyiwa mahojiano zaidi ambapo serikali itajua nini la kufanya hapo baadae.
Alisema wanalazimika kulifanyia kazi suala hilo, kwa vile tayari imetolewa tahadhari ya kutokea balaa litakalowahusisha watu wengi.


No comments:

Post a Comment