VIDEO Queen wa Bongo, Agnes Gerald
‘Masogange’ alitarajiwa kutua nchini juzi Jumatano akitokea Afrika
Kusini huku siri nzito ya mzigo aliodakwa nao ikitawala, Amani
linakujuza.
Masogange anakuja Bongo baada ya
kumaliza kulipa deni lote la randi 30,000 (shilingi milioni 4.8)
alizoamriwa kulipa na Mahakama Kuu ya Gauteng iliyopo Kempton Park
jijini Johannesburg nchini humo baada ya kumtia hatiani kwa kosa la
kuingiza kemikali haramu, Julai 5, mwaka huu.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika,
Masogange anarejea na Melisa Edward ambaye alikamatwa naye lakini
mahakama ikamwona hana hatia.
SIRI NZITO
Ujio wa Masogange bado una siri nzito
kwani licha ya mahakama hiyo kumtia hatiani kwa faini au kifungo cha
miezi thelathini jela, lakini bado serikali ya Tanzania inahaha kutaka
kujua mzigo aliodakwa nao alitumwa na nani!
“Masogange ameahidi kutowataja watu waliompa mzigo akidai kuwa itaendelea kuwa siri yake mpaka anakufa,” kilipasha chanzo chetu.
WATOTO WA VIGOGO
Watoto wa vigogo ndiyo wamekuwa
wakitajwa zaidi kuhusika na kumtuma Masogange ingawa hakuna jina la moja
kwa moja la mtoto yeyote wa kigogo lililowahi kutajwa.
ANAYEMJUA MWAKYEMBE
Mpaka sasa, Serikali ya Tanzania kupitia
kwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison George Mwakyembe iliwahi kumtaja
kijana aitwaye Mangunga ambaye ndiye anadaiwa kuwa na Masogange ndani ya
ndege kwenda Afrika Kusini.
Mwakyembe aliamuru kijana huyo asakwe na
kukamatwa ili kujibu mashitaka ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya
Methamphetamine kwa Tanzania huku Afrika Kusini ikisema unga huo ni
ephedrine ambao si wa kulevywa bali ni kemikali haramu.
KAMATI YA MAPOKEZI YAMWANDALIA PATI YA MAMILIONI
Habari za kifukunyuku zinadai kuwa,
jijini Dar baadhi ya mastaa wameunda kamati ya mapokezi ya Masogange,
Jacqueline Wolper Massawe akiwa mwenyekiti wake, katibu na wajumbe
hawakupatikana majina.
KAZI YA KAMATI
Kazi ya kamati hiyo inadaiwa ni
kukusanya mamilioni kutoka kwa mapedeshee wa mjini ili kuwezesha
kufanyika kwa pati ya nguvu ya kumshukuru Mungu kwa kumsaidia staa huyo
kutoka jela na kurudi Bongo.
“Kamati iko chini ya uenyekiti wa
Wolper, si unajua huyu dada hata hivi karibuni alimfanyia birthday
Masogange japo mwenyewe hakuwepo?
“Sherehe itaandaliwa kwenye ukumbi mmoja
uliopo ufukweni mwa Bahari ya Hindi lakini kwa sasa sitautaja ili
kuepuka wazamiaji,” kilisema chanzo chetu.
NZOWA: HIYO PATI ITAFANYIKIA WAPI, SINZA KWA DADA’KE AU?
Kufuatia kuwepo kwa madai kwamba,
Masogange akitua tu Bongo atadakwa na Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na
Madawa ya Kulevya Tanzania, juzi Amani lilimsaka kamanda wa kikosi
hicho, Godfrey Nzowa na kumuuliza kuhusu madai hayo.
Amani: Afande, naomba unisaidie mawili
matatu. Yule msanii Masogange aliyekamatwa na madawa ya kulevya na
kuhukumiwa Afrika Kusini anarejea nchini kesho Jumatano (jana) Je, ninyi
mna mpango wowote wa kumkamata akitua?
Nzowa: Sisi hatuna shida naye tena. Alishahukumiwa kule, sasa tumkamate huku kwa sheria gani?
Amani: Basi kuna habari kwamba mmepanga
kumkamata maana tumeambiwa na chanzo chetu kuwa atafanyiwa pati ya
kumshukuru Mungu kwa kumtoa katika mazito.
Nzowa: Hiyo pati ataifanyia wapi, Sinza kwa dada’ke au?
Amani: Bado hawajaweka wazi.
Nzowa: Sisi hatuna shida naye.
WOLPER ASAKWA KUULIZWA
Juzi asubuhi, Amani lilimtafuta Wolper
kwa njia ya simu yake ya mkononi na kumuuliza ukweli wa kuwepo kwa
kamati ya sherehe ya mapokezi ya Masogange ambapo alijibu:
“Nipo shooting (narekodi) Arusha, nitawatafuta baadaye kuhusu hilo suala kama lipo au halipo.”
MASOGANGE NAYE
Juzi Jumanne, Amani lilimpigia simu Masogange akiwa Afrika Kusini na kumuuliza kuhusu ujio wake wa jana.
Masogange: Ni kweli narudi huko (Bongo) Jumatano, mipango yote ya safari tayari, namshukuru Mungu kwa yote.
WENGINE WANASOTA!
Wakati Masogange akiwa ameponea tundu la
sindano, mrembo mwingine wa Bongo Fleva, Sandra Khan ‘Binti Kiziwi’
anateseka gerezani huko China alipofungwa kwa miaka mitatu kwa msala wa
madawa ya kulevywa wakati Saada Kilongo yuko mahabusu Bongo kwa kesi ya
aina hiyohiyo.
No comments:
Post a Comment