PICHA za chumbani za mwigizaji Rose Ndauka na mchumba wake, Malick
Bandawe zimevuja baada ya rafiki wa karibu wa wapenzi hao kuzisambaza
kitaani.
Rafiki
huyo wa karibu alizungumza na Weekly Star Exclusive na kusema kuwa
wapendanao hao walikuwa wakilala katika hoteli moja iliyopo maeneo ya
Mbezi Beach, jijini Dar kwa ajili ya kuilea mimba aliyonayo bibie.
“Huwa wanalala kwenye hoteli tangu mimba ilipoanza kuonekana, kusema
kweli Malick anamlea Rose kama yai wasiwasi wangu atamlemaza wakati
mjamzito anatakiwa afanye mazoezi,” alisema rafiki huyo kwa sharti la
kutochorwa gazetini.
Baada ya kupata ‘ubuyu’ huo, Weekly Star
Exclusive ilimuendea hewani Malick na kumuuliza juu ya picha hizo na
suala la kuhamisha maskani hotelini hapo kama ni la kudumu au la!
Alitiririka:
“Ni kweli nyumbani tunaenda mara mojamoja kwa sababu
nahitaji mchumba wangu asiwe na msongo wowote wa mawazo, anahitaji
sehemu ambayo imetulia ili ujauzito nao utulizane, muda mwingi
tunautumia hotelini zaidi,” alisema Malick.
No comments:
Post a Comment