KATIKA miaka hii kumekuwa na utaratibu
Party wa kuwahusisha mashoga.
Kutokana na utaratibu huo usiofaa kumefanya
Kutokana na utaratibu huo usiofaa kumefanya
sherehe hizo kupoteza uhalisia.
Kwa tafsiri nyepesi, Kitchen Party ni
Kwa tafsiri nyepesi, Kitchen Party ni
sherehe ambayo hufanyika kwa lengo maalumu
la kumpa vyombo vya jikoni binti
anayekaribia kuingia kwenye ndoa kwa
maana ya kuolewa.
Sherehe hii huambatana na mwaliko wa ndugu,
Sherehe hii huambatana na mwaliko wa ndugu,
jamaa na marafiki. Lakini pia huwa maalumu
kwa ajili ya wanawake.
Lakini cha kushangaza hizi sherehe
Lakini cha kushangaza hizi sherehe
zimekuwa ni uwanja wa kualika wanaume
wanaojifanya wanawake 'mashoga' ambao
hufanya mambo ya aibu.
Mengine ni aibu kiasi cha kutotamkika,
Mengine ni aibu kiasi cha kutotamkika,
lakini ninaposikia au kuona hayo kwenye
sherehe hizi huwa ninajisikia kichefu
chefu.
Mashoga hawa hutumika kuonyesha mambo
Mashoga hawa hutumika kuonyesha mambo
ambayo kimaadili hayapaswi kuonekana
hadharani.
Mfano wa mambo ambayo kwa ufahamu wangu
Mfano wa mambo ambayo kwa ufahamu wangu
ninaona hayafai kuonekana hadharani, ni
pamoja na kukata viuno hadharani, kuvua
nguo na wakati mwingine hata kuonyesha
namna tendo la ndoa linavyofanyika.
Wakati sisi tunakua ilikuwa ni mwiko
Wakati sisi tunakua ilikuwa ni mwiko
mwanamke au mwanaume akikata viuno
hadharani kutokana na unyeti wa tendo
lenyewe. Lakini leo hii mambo haya
ovyo, kiasi kwamba hata unapokwenda
dukani unamnong'oneza muuzaji ambaye
naye huitoa kwa kificho isionekane.
Lakini leo hii utamkuta mama mtu mzima
mwenye maumbile makubwa nyuma akiwa
amemtanguliza shoga mbele huku anakata viuno
huku, kaning'iniza nguo za ndani nje nje
bila wasiwasi.
Ninaugua juu ya hilo kwa sababu ni
Ninaugua juu ya hilo kwa sababu ni
vitendo vya aibu ambavyo havifuati
maadili ukizingatia washiriki wanaweza
kuwa mama, dada au shangazi zetu hivyo
suala la rika huwa halizingatiwi.
Mbali ya hayo, ninachelea kusema kuwa
Mbali ya hayo, ninachelea kusema kuwa
mambo ambayo huonyeshwa na mashoga
hao, huwa ni aibu.
Ukiangalia jinsi anavyofanya shoga na
Ukiangalia jinsi anavyofanya shoga na
yeye ni mwanaume, ni aibu kwetu sisi
wanawake kwa sababu wanaonekana ni wajuzi
zaidi, hivyo wanawake huwa tunajitukanisha
pasipo kujijua.
Jingine la kushangaza zaidi ni pale
Jingine la kushangaza zaidi ni pale
tunapokuwa mstari wa mbele katika
kushabikia mambo ambayo hayana maana,
tena kwa shangwe na vigelegele tukionyesha kufurahia mambo hayo.
Kwa upeo wangu, wakati binti anakaribia
Kwa upeo wangu, wakati binti anakaribia
kuolewa kuna mafunzo ya ndani kabisa
ambayo hupewa na bibi, shangazi au somo
ambaye ni maalumu kwa ajili ya kumfundisha
namna ya kumtunza mume, usafi na kutunza
familia pindi atapoingia kwenye ndoa yake.
Na baadaye sherehe za Kitchen Party
Na baadaye sherehe za Kitchen Party
hufuatia
maalumu kwa ajili ya kumzawadia vyombo
vya jikoni sambamba na kuhitimisha kwa
sherehe za kuagwa rasmi na familia, ndugu
jamaa na marafiki.
Huo ndiyo utaratibu ninaoufahamu mimi.
Huo ndiyo utaratibu ninaoufahamu mimi.
Lakini leo hii utaratibu huu umebadi
lishwa kiasi cha Kitchen Party kuwa
mahali ambako hufanyika vitendo vinavyo
chochea vitendo vya kisagaji, ushoga,
ulevi, matusi ya nguoni na wakati
mwingine hata ugomvi.
Binafsi sipendezwi na hili kwakuwa lengo
Binafsi sipendezwi na hili kwakuwa lengo
ni kujenga na si kubomoa. Je, kizazi
kilichopo na kijacho kinajifunza nini?
Na inakuwaje kinamama watu wazima ndio
Na inakuwaje kinamama watu wazima ndio
wanakuwa mashabiki wa mambo yasiyo ya
msingi? Je, mmerogwa au mnajitoa ufahamu?
Ni lazima kuita mashoga?
Ifike mahali tuwe na hofu ya Mungu kwa
Ifike mahali tuwe na hofu ya Mungu kwa
kuzingatia maadili kwa maana ya kwamba
wanawake tunaweza, na hatuna haja ya
kuita mashoga wanogeshe Kitchen Party
ilihali si mahali sahihi kwao.
chanzo:daima.
chanzo:daima.
No comments:
Post a Comment