Wadau
na mashabiki wa mastaa wawili nchini, Wema Sepetu wa Bongo Movie na
Nasibu Abdul ‘Diamond’ wa muziki wa kizazi kipya, wamebariki ndoa ya
wapenzi hao kwa kusema kuwa ni watu wanaoendana na kutegemeana kwa kiasi
kikubwa.
Mwanzoni mwa wiki hii, Wema na Diamond walitupia katika kurasa zao za
mitandao ya kijamii picha zao, ambazo zinaonekana zilipigwa eneo moja
kwa simu moja na hivyo kuwapa wakati mzuri mashabiki wao ambao
walionekana kupendezwa na uhusiano wao na kupendekeza waoane.
“Hii
ndiyo couple bomba zaidi ya wasanii Bongo, kwa nini msioane? Mnapendeza
sana jamani, ebu Diamond Platnumz achana na Penny bwana, huendani naye
kwanza kuna mambo ya dini na nini…,” aliandika shabiki mmoja.
No comments:
Post a Comment