Msanii anayeng’ara kwenye filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ juzikati aliwaacha midomo wazi watu baada ya kwenda kuchukua msosi mara tatu kwenye shughuli iliyochukua nafasi ndani ya Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar.
Lulu
alikuwa kati ya wasanii waliofika eneo hilo kushiriki katika harambee
ya kansa ya wanawake iliyoendeshwa na taasisi ya kuzuia kansa nchini
ambapo baada ya zoezi hilo, waalikwa walijongea eneo la maakuli.
Huku akionekana mwenye ‘ubao’, Lulu alikwenda kwenye foleni na kuchukua pleti ya kwanza, akaifuta kisha akanyanyuka na kwenda kuchukua nyingine, nayo akaimaliza, baada ya muda akaenda kuchukua nyingine ambapo haikufahamika kama nayo aliifuta au alisaidiwa na mtu.
Akilizungumzia tukio hilo, Lulu aliliambia Ijumaa: “Nakula sana na hii ni kawaida yangu, najua watasema lakini kwenye msosi huwa sikai nyuma.”
Huku akionekana mwenye ‘ubao’, Lulu alikwenda kwenye foleni na kuchukua pleti ya kwanza, akaifuta kisha akanyanyuka na kwenda kuchukua nyingine, nayo akaimaliza, baada ya muda akaenda kuchukua nyingine ambapo haikufahamika kama nayo aliifuta au alisaidiwa na mtu.
Akilizungumzia tukio hilo, Lulu aliliambia Ijumaa: “Nakula sana na hii ni kawaida yangu, najua watasema lakini kwenye msosi huwa sikai nyuma.”
No comments:
Post a Comment