Blogger Widgets

October 18, 2013

Msanii Elizabeth Lulu Atia Aibu Tena Ndani ya Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar


Msanii anayeng’ara kwenye filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ juzikati aliwaacha midomo wazi watu baada ya kwenda kuchukua msosi mara tatu kwenye shughuli iliyochukua nafasi ndani ya Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar.
Lulu alikuwa kati ya wasanii waliofika eneo hilo kushiriki katika harambee ya kansa ya wanawake iliyoendeshwa na taasisi ya kuzuia kansa nchini ambapo baada ya zoezi hilo, waalikwa walijongea eneo la maakuli.
Huku akionekana mwenye ‘ubao’, Lulu alikwenda kwenye foleni na kuchukua pleti ya kwanza, akaifuta kisha akanyanyuka na kwenda kuchukua nyingine, nayo akaimaliza, baada ya muda akaenda kuchukua nyingine ambapo haikufahamika kama nayo aliifuta au alisaidiwa na mtu.

Akilizungumzia tukio hilo, Lulu aliliambia Ijumaa: “Nakula sana na hii ni kawaida yangu, najua watasema lakini kwenye msosi huwa sikai nyuma.”

No comments:

Post a Comment