Blogger Widgets

October 20, 2013

Msanii Nisha Atia Fola

Actress maarufu nchini Salma Jabu(Nisha) amesema kuwa aliingia katika muziki wa Bongofleva kwa kufuata mkumbo baada ya kuwaona waigizaji wenzake wengi wakiingia katika muziki na yeye ndiyo akajitumbukiza na matakeo yake kukaa sana kimya na kupotea katika fani hiyo. Nisha amesema kuwa hatathubutu tena kufuata mkumbo kwenye fani nyingine bali yeye ameamua kujikita zaidi
kwenye fani yake ya filamu. Akizungumza na Gpl star huyo wa filamu za Red-Cross, Matilda, Pusi Na Paku na Tikisa alisema "Niliona waigizaji wanaingia kuimba na mimi nikaingia, nilivamia fani tu ndiyo maana  najuta, nimeamua nikae chonjo kwanza na mambo hayo nijikite zangu kwenye filamu"

No comments:

Post a Comment