Actress maarufu nchini Salma Jabu(Nisha) amesema kuwa aliingia katika
muziki wa Bongofleva kwa kufuata mkumbo baada ya kuwaona waigizaji
wenzake wengi wakiingia katika muziki na yeye ndiyo akajitumbukiza na
matakeo yake kukaa sana kimya na kupotea katika fani hiyo. Nisha amesema
kuwa hatathubutu tena kufuata mkumbo kwenye fani nyingine bali yeye
ameamua kujikita zaidi
kwenye fani yake ya filamu. Akizungumza na Gpl
star huyo wa filamu za Red-Cross, Matilda, Pusi Na Paku na Tikisa
alisema "Niliona waigizaji wanaingia kuimba na mimi nikaingia, nilivamia
fani tu
ndiyo maana najuta, nimeamua nikae chonjo kwanza na mambo hayo nijikite
zangu kwenye filamu"
No comments:
Post a Comment