Ufoo Saro wakati akitolewa chumba cha upasuaji kupelekwa wodini.
Baadhi ya waandishi na wananchi wakiwa wamekusanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kujua hali ya Ufoo.
Mtangazaji wa ITV na Radio One, Ufoo Saro amefanyiwa upasuaji baada
ya kujeruhiwa vibaya kwa risasi na mzazi mwenziye aitwaye Anther Mushi
mapema leo. Upasuaji huo umefanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
kuanzia asubuhi mpaka saa 12 jioni. Ufoo alipigwa risasi akiwa nyumbani
kwa mama yake mzazi Annastazia Saro baada ya kutokea mgogoro baina yake
na mzazi mwenziye. Katika tukio hilo, Anther alimpiga risasi na kumuua
mama Ufoo kisha na yeye akajilipua kwa risasi baada ya kumpiga risasi
Ufoo. Kwa sasa Ufoo amehamishiwa katika wodi ya Kibasila anapoendelea
kupatiwa matibabu. Umati wa watu ulikusanyika katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili kuanzia asubuhi ili kujua hali ya mtangazaji huyo.
From:GPL