Blogger Widgets

October 22, 2013

Picha Zikonesha Jinsi Juma Kaseja na Uhuru Selemani walivyohudhuria Kwenye Mechi Kati ya Simba Na Yanga


KASEJA (MWENYE KOFIA) AKIFUATILIA MECHI UWANJA WA TAIFA. MBELE YAKE MWENYE NYWELE ZENYE RANGI NI UHURU SELEMANI

Katika kipindi cha miaka kumi sasa, kipa wa zamani wa Simba, Juma Kaseja aliingia kwa mara ya kwanza Uwanja wa Taifa kama shabiki.

Kaseja aliyekuwa nahodha wa Simba, aliachwa katika kikosi hicho kwa madai ya kushuka kiwango ingawa kila kitu kinaonyesha zilikuwa ni chuki binafsi.
Katika mechi ya jana iliyomalizika kwa sare ya mabao 3-3, Kaseja alionyesha vitu kadhaa muhimu ambavyo vinaweza kuelezewa.

Pamoja na kuachwa kwa chuki binafasi, lakini alionyesha hana chuki na Simba na kwenda kukaa katika jukwaa la mashabiki wa Simba.

Achana na hivyo, Kaseja alizidi kuonyesha yeye ni Simba damu kwa kuwa kama ingekuwa tofauti angeweza kwenda kukaa jukwaa la Yanga aliyowahi kuichezea kwa mwaka mmoja.

Tatu, akiwa na Uhuru Selemani ambaye pia aliwahi kuichezea Simba, Kaseja alionekana si mpenda makuu kwani alikaa sehemu ya kawaida na akaonyesha utulivu si kama walivyo wachezaji wengine nyota.

Wakati Simba ikishindiliwa mabao katika kipindi cha kwanza alionekana kama alikuwa anawaza kitu fulani, angalau katika kipindi cha pili, tabasamu lake lilianza kuonekana.

No comments:

Post a Comment