Baadhi ya wananchi walionaswa katika msako wa biashara haramu ya ukahaba. Pichani ni wauzaji na wanunuzi.
MZEE mmoja
aliyejitambulisha kwa jina la Abdullahimu Mnami (48) amenaswa akiendesha
gesti bubu kinyume cha sheria za nchi.Tukio hilo lilitokea Oktoba 26,
mwaka huu maeneo ya Tuangoma jijini Dar, baada ya waandishi wetu
kuzinyaka taarifa hizo na kuzifikisha kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa
huo, Chande Mohammed aliyefika eneo hilo na polisi.Awali, ili
kujiridhisha, mmoja wa mapaparazi wetu alijifanya mteja na kufika katika
gesti bubu hiyo, kisha kupangisha chumba kwa malazi ya siku moja kwa
malipo ya shilingi 3000 tu lakini pasipo kuandikisha mahali popote.
Akizungumza
na waandishi wetu mbele ya maaskari na mwenyekiti, mzee huyo alisema
alishindwa kuisajili gesti yake kwa kuwa haikuwa na viwango
vinavyokubalika na manispaa (ya Temeke).
“Ningefuata
utaratibu, manispaa isingeniruhusu kutokana na ubora wa vyumba
vyenyewe, kama mnavyoona. Pia njaa tu jamani ndiyo imenifanya nianzishe
gesti hii,” alisema mzee Abdullahim.
Hata
hivyo mwenyekiti wa mtaa huo, alisema kuwa mzee huyo ana kesi ya kujibu
kwa kukiuka taratibu za kibiashara zilizowekwa na halmashauri na
kumuamuru aifunge gesti hiyo mara moja huku akiahidi kumpeleka Baraza la
Kata kwa ajili ya masikilizano ya awali.
Timu yetu
iliwaachia msala wao na kuendelea na oparesheni nyingine ambapo
walifanikiwa kuwanasa machungudoa wakijiuza jirani na mtaa huo huku
ikielezwa kuwa, wateja wa madadapoa hao hupelekwa katika gesti bubu ya
mzee huyo kwa vile ni bei poa.
From:Gpl
No comments:
Post a Comment