Muimbaji mkongwe nchini Nguza Viking aka Babu Seya na mwanaye
Papii Kocha, wataendelea na kifungo cha maisha jela baada ya mahakama ya
rufani nchini kuitupilia mbali rufaa yao iliyosikilizwa leo.
Babu Seya na Papii Kocha walihukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka
2004 baada ya kupatikana na hatia ya kuwanajisi watoto wa shule ya
Msingi, Mashujaa, Sinza jijini Dar es Salaam.
Wawili hao wamewahi kukata rufaa tena na hawakufanikiwa na hukumu hii
ya rufaa ni ya mwisho kusikilizwa. Katika rufaa hiyo wakili wa Babu
Seya na Papii Kocha alikuwa akiiomba mahakama hiyo ifute ushahidi na
waachiwe huru.
No comments:
Post a Comment