Kila tarehe 16nov hua ni siku ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa ndugu yetu/mpendwa wetu Albert Mangwea,ambae alizaliwa huko songea mwaka 1982.Baadae wazazi kuhamia morogoro. Shughuli ya kukumbuka siku yake ya kuzaliwa imeambatana na siku ya kuhitimisha msiba yaani 40,katika kuelekea siku hii nyumbani kwao kihonda mkoani morogoro waliandaa misa ya kumuombea ambayo ilianza na mkesha wa tarehe 15 kuamkia 16 hizi ni picha za usiku wa mkesha nyumbani kwao albert.
Hawa ni miongon wa waliohudhuria akiwemo Bdozen toka xxl ya cloudsfm,Young Dee na Dj venture
Asubuhi kulipokucha tulielekea kanisani ambalo lipo barabara ya kuelekea Dodoma kanisa la ROMAN CATHOLIC mtakatifu Monica parokia ya Kihonda,Misa ilianza sa 1 asubuhi na iliongozwa na paroko wa kanisa hiloPadri OCTAVIAN MSIMBE.
Asubuhi kulipokucha tulielekea kanisani ambalo lipo barabara ya kuelekea Dodoma kanisa la ROMAN CATHOLIC mtakatifu Monica parokia ya Kihonda,Misa ilianza sa 1 asubuhi na iliongozwa na paroko wa kanisa hiloPadri OCTAVIAN MSIMBE.
Misa
ilipokamilika waumini wote tulisogea eneo alipolala mpendwa wetu ALBERT
MANGWEA,ambapo tulipofika eneo la makaburini tulianza kwa kuelekea
kaburi alilolala baba mzazi wa ALBERT MANGWEA mzee KENETH MANGWEA bbada
ya misa kukamilika tulihamia kaburi alilolala mpendwa wetu/ndugu
yetuALBERT MANGWEA ambalo lipo mita chache na la BABA.
Misa
ikiendelea kwenye kaburi la marehemu mzee KENETH MANGWEHA baba mzazi wa
Marehemu Ngwea.Mara baada ya kukamilika kwa misa kwenye kaburi la mzee
Keneth waumini wote tuliokuwa makaburini tulisogea kwenye kaburi
alilolala mpendwa wetu MANGWEA
Waombolezaji
wakifatilia ibada.Misa ilipoisha watu wengi waliokua karibu,wapendwa wa
ALBERT hawakuondoka mapema makaburini ndugu/mzazi walitangulia nyumbani
lakini watu wengi waliokaribu waliendelea kuwa makaburin wakiwasha
mshumaa kama ishara ya kumkumbuka mpendwa wetu na kumsalia huko aliko
apumzke kwa aman
Kutoka
kushoto ni M2the p,Darkie Master,Quick Rocker,Dj Venture na Dulah
spatan,na kulia ni Bdozen,Geez Mabovu na nndugu waliokua karibu na
ngwair wakisali kwenye kaburi la mpendwa ALBERT MANGWEA.
Darkie
Master akipiga saluti kwenye kaburi la Ngwea.Baada ya kuwasha mishumaa
na kuweka mashada ya maua,kilichofuata zilikua zikisikika nyimbo za
Marehem ngwea ambazo zilikua zikipigwa kutoka kwa gari ya maneck nyimbo
hizo ni zile ambazo hazikutoka japo zipo tayari studio,watu waliokua
eneo hili ni pamoja na Quick Rocker,Maneck,Bdozen,Young Dee,Dark
master,Geez mabovu,Dj venture[ambae aliwahi kuwa meneja wa ngwea]Dulah
spatan,ndg Muro junior Aliyekua meneja wa Ngwea had kipindi cha mwisho
,Jordan moja ya wadogo wa ngwea kimuzik aliokua akiwasimamia chin ya
lebel yao ya DENJAVUU MUSIC.
No comments:
Post a Comment