Akizungumza
na gazeti la Uwazi juzi, Marando alisema kazi aliyokusudia kuifanya
ameimaliza, sasa anasubiri majaji waliosikiliza alichokisema ili watoe
uamuzi wa mwisho lakini pia anamtegemea Mungu.
“Mimi
kazi nimemaliza sasa nawasubiri hao wakubwa (majaji) ili wapime
nilichowaambia kwa mujibu wa sheria na kisha watoe uamuzi, lakini pia
namtegemea Mungu,” alisema Marando.
Alisema
ameiomba Mahakama ya Rufaa Tanzania ifanye marejeo kuhusu hukumu
iliyoitoa na ifute ushahidi uliowatia hatiani wateja wake hao na adhabu
ya kifungo cha maisha jela wanayoitumikia kwa sasa.
Alipoulizwa
alitumia muda gani kuwasilisha hoja zake hizo, Marando alisema takriban
dakika 120 mbele ya jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo, wakiongozwa
na Jaji Nathalia Kimaro akisaidiana na Jaji Mbarouk Mbarouk na Jaji
Salum Massati.
Akiwa
mahakamani hapo, Marando alidai kuwa mahakama iliteleza katika kutoa
uamuzi uliowatia hatiani na kuwafunga maisha wateja wake na kwamba
kuteleza huko kunaonekana waziwazi.
Alifafanua
kuwa wakati wakifanya majumuisho ya kesi hiyo, mahakama ilijiridhisha
kwamba kulikuwa na makosa katika kupokea ushahidi wa watoto wanaodaiwa
kufanyiwa vitendo hivyo.
Alidai kuwa ushahidi wa watoto hao ulichukuliwa bila ya kufuata taratibu za uchukuaji wa ushahidi wa watoto.
Alieleza
kuwa mtoto anayesoma shule kuanzia ya msingi anapotoa ushahidi licha ya
tahadhari, ana uwezo wa kutambua zuri na baya na kwamba lazima ushahidi
wake uwekwe kwenye kumbukumbu ya maandishi na kwamba usipoonekana
ushahidi wote ni batili na unaondolewa.
Katika
shauri hilo upande wa Mkurugenzi wa Mashtaka uliwakilishwa na Mawakili
Jackson Mlaki, Angaza Mwaipopo, Emakulata Banzi, Joseph Pande na Apimack
Mbarouk ambao waliyapinga maombi hayo kuhusu marejeo kwa madai kuwa
yamepelekwa mahakamani bila usahihi.
Mahakama hiyo imesema itatoa uamuzi wake siku itakayotangaza.
Babu
Seya na Papii Kocha wako jela kwa makosa 10 ya kubaka watoto wa kike
wenye umri kati ya miaka sita na minane na mengine 11 ya kulawiti watoto
wa kike wenye umri kama huo.
Walidaiwa kutenda makosa hayo kati ya Aprili na Oktoba 2003 eneo la Sinza Kwaremy jijini Dar es Salaam.
Katika kesi hiyo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka ambaye alishitakiwa kwa makosa mawili ya kumsaidia Babu Seya kutenda makosa hayo kwa kuwaruhusu baadhi ya wanafunzi hao kutoka madarasani, aliachiwa huru na Mahakama ya Kisutu.
Katika kesi hiyo, Mwalimu wa Shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka ambaye alishitakiwa kwa makosa mawili ya kumsaidia Babu Seya kutenda makosa hayo kwa kuwaruhusu baadhi ya wanafunzi hao kutoka madarasani, aliachiwa huru na Mahakama ya Kisutu.
No comments:
Post a Comment