RAIS wa Wasafi Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati alifunguka
kuwa kwenye maisha yake ya ndoa atakayoingia siku chache zijazo,
aliyekuwa mchumba wake wakamwagana na kurejeana hivi karibuni, Wema
Sepetu asitegemee kuolewa naye. Diamond ambaye ni staa wa Bongo Fleva
aliyasema hayo mbele ya mwandishi Novemba 7, mwaka huu jijini Dar
kufuatia kuulizwa anamchagua nani wa kumuoa kati ya Wema Sepetu na
mchumba wake wa sasa, Penniel Mungilwa ‘Penny’.Swali kwa Diamond
liliibuka baada ya kuzagaa kwa tetesi kwenye mitandao ya kijamii kwamba
yu mbioni kumvisha pete ya uchumba mmoja wa mademu zake.
Swali
hilo lilimfanya Diamond afunguke kwa kusema kwamba anachokijua yeye na
ambacho kipo kwenye mikakati yake, mke wake mtarajiwa ni Penny.
“Najua
wengi wanahisi mimi ninaweza kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kutokana na
dini yangu kuruhusu lakini jambo hilo mimi silifikirii hata kidogo kwa
kuwa kwenye maisha yangu nilishapanga nitaoa mke mmoja tu,” alisema
Diamond.
Akaendelea:
“Watu wanasema mengi juu yangu na Wema, wengi wao hawajui nafsi yangu
inataka mwanamke yupi, ninachoweza kusema na watu wakasikia na kunielewa
basi wajue kwamba Penny ndiye mke wangu, Wema asitegemee kuolewa na
mimi.”
Diamond
alikwenda mbele zaidi kwa kumwanika Penny kwamba ana sifa ya kuwa mke
kwani ni mvumilivu sana na anaonesha upendo wa dhati kwake.
“Kwa
maana hii basi hakuna mwanamke mwenye jina kubwa wala sura nzuri zaidi
ya Penny ninayeweza kumwita mke wangu. Najua kila mtu ana namna yake ya
kuchagua ampendaye, ndiyo maana utaona watu wanasema hili mara lile,
lakini hawajui nafsi yangu inataka mwanamke wa aina gani,” alisema
Diamond na kuongeza:
Kama kuna
demu anayejipa matumaini hayo basi asitegemee hata siku moja kwa sababu
kuoa kwangu kutazingatia mke mwema na si bora mke, Penny pekee ndiye
mwenye sifa za kuwa mke wangu,” alisema Diamond.
No comments:
Post a Comment