Katika hatua nyingine, imedaiwa kuwa Lady Gaga ameachwa na mpenzi wake Taylor Kinney. Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, uhusiano kati ya Gaga na muigizaji huyo umekuwa matatani kwa miezi kadhaa kutokana na Lady Gaga kuwa busy kupitiliza.
‘Taylor amemuambia Gaga kuwa ameolewa na kazi yake na hawezi kuwa na uhusiano na staa huyo pamoja na jinsi anavyohangaika kujionesha,’ chanzo kimoja kililiambia gazeti hilo.
‘Anampenda sana lakini humuona kwa nadra sana. Gaga huwa hasimami kufanya kazi- huandika nyimbo akiwa anaoga na huota nguo mpya za kuvaa akiwa amelala.’
Kinney, 32, anasemekana kuchanganyikiwa na kuwa peke yake mara nyingi na muda mchache wa kukaa na Gaga, ambaye mara zote huwa amezungukwa na wasaidizi kibao pamoja na walinzi. Wapenzi hao huwa na usiku mmoja tu ndani ya mwezi mzima wa kuwa pamoja.
From:Bongo5
No comments:
Post a Comment