Blogger Widgets

November 4, 2013

Picha zikionesha jinsi Khadija Kopa Akifanya Show YakeYa Kwanza Ndani ya Dar Live Hii ni Baada ya Kukaa Miezi Minne Ndani kwa Kifiwa na Mume wake na Kupewa Million Moja Kama Eda


MALKIA wa Mipasho Khadija Kopa, usiku wa kuamkia  leo ameibuka kwa mara ya kwanza na wimbo mpya uitwao 'A Lady with Confidence' katika kiwanja cha burudani cha Dar Live, ikiwa ni mara yake ya kwanza kuimba baada ya kukaa ndani eda kwa muda wa miezi minne na siku 10. Wimbo huo, ambao unaonekana kuwa moto wa kuotea mbali, ameuimba katika onesho lake maalumu la kumtoa nje na umemuwezesha pia kupewa kitita cha shilingi milioni moja na uongozi wa Dar Live, pesa iliyokabidhiwa kwake na Mkurugenzi wa Dar Live na Global Publishers, Masha Jame
 
Malkia wa mipasho Khadija Kopa akiwa stejini ndani ya Usiku wa Kumtoa Malkia, Dar Live.
 
Pichani juu ni malkia wa mipasho Khadija Kopa akiwa stejini katika usiku wake maalumu, huku akisindikizwa na kundi zima la TOT.

 
Kiongozi wa TOT, Gasper Tumaini, akiushukuru uongozi wa Dar Live kwa kuandaa usiku wa Malkia muda mfupi kabla hajapanda stejini.
Mkurugenzi wa Dar Live Masha James (kushoto) akimkabidhi Kopa bahasha yenye kitita cha shs milioni moja usiku wa kuamkia leo ndani ya Usiku wa Kumtoa Malkia, Dar Live.

From:GPL

No comments:

Post a Comment