Sasa
hivi ukisafiri nchi za nje na ukakutana na ukaguza wa kuzidi kiwango
cha kawaida katika viwanja vya ndege wala usishangae, sababu biashara
haramu ya dawa za kulevya inazidi kushamiri na kusababisha vyombo vya
usalama vizidi kuwa makini katika udhibiti.
Hivi karibuni maafisa wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Trudeu huko
Montreal, Canada wamemkamata mwanamke mmoja aliyejaribu kupitisha dawa
za kulevya aina ya Cocaine zilizofichwa ndani ya maboga matatu.
Maafisa usalama wa uwanja huo wamesema walimtilia mashaka abiria
huyo mwanamke aitwaye Mercedes Jerez Farias (26) kutokana na maboga
hayo kuwa na uzito zaidi ya ule wa kawaida kwa maboga ya ukubwa huo.
Mashine ya ukaguzi wa mizigo uwanjani hapo ulithibitisha kuwa maboga hayo yalikuwa na dawa za kulevya ndani.
No comments:
Post a Comment