Blogger Widgets

November 8, 2013

UNIVERSITY LENS:Picha Ya Wanafunzi wawili wa CBE DODOMA waliofariki Baada ya Kupata Ajari ya Pikipiki

 

Miili ya Marehemu Ramadhan Lesso na Gerge Lwandala inaonakana kabla ya kuondolewa katika kijiji cha Ihumwa barabara ya Morogoro Dodoma kabla ya kuondolewa na kuhifadhiwa katika chumba cha maiti hospital ya mkoa. 

Baadhi ya watu wakiisogeza miili ya Wanafunzi wa CBE Dodoma  waliokufa kutokana na kuligonga tela la lori kwa nyuma kutokana na mwendo kasi huku lori hilo likiwa limetelekezwa zaidi ya wiki bila alama yoyote barabarani hapo.  

Baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), walionekana kujaribu kutoa msaada katika ajali hiyo iliyosababisha vifo vya wanafunzi wa chuo cha biashara CBE Dodoma. 

Askari wa wasalama barabarani akisaidiana kupima upana wa barabara sehemu ilipotokea ajali hiyo ilihusisha pikipiki na lori la mizigo.

Na John Banda, Dodoma

WANAFUNZI wawili wa chuo cha biashara  wamepoteza  CBE wamekufa papo hapo kwenye ajali baada ya kugonga tela la mizigo lililokwama barabarani baada ya kuhalibika.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 1.00 usiku baada ya kugonga tela la lori la mizigo kwa nyuma wakati wanafunzi hao walipokuwa wakitokea kwenye mwaliko wa sherehe ya rafiki zao iliyofanyika katika kijiji cha ihumwa manispaa ya Dodoma.

Gazeti hili lilishuhudia msongamano mkubwa wa magari katika barabara hiyo iliyopo pembezoni mwa kambi ya jeshi ya Ihumwa kwa takribani saa zaidi ya tatu kabla ya polisi wa usalama barabarani kufika na kuongoza utaratibu wa kuondoka.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Suzan Kaganda alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa wanafunzi hao wakati wakiendesha pikipiki hiyo  yenye namba za usajili T 420 CCN  waliokuwa wakukitokea barabara ya morogoro kuingia mjini.

Suzan aliwataja kuwa ni Ramadhan Lesso na Gerger Lwandala wanafunzi wa CBE  na kwamba uzembe wa Dereva wa lori hilo lenye namba za usajili T 477 ABM na huku Tela lake ni T 838 AAZ aliyeliacha barabrani zaidi ya wiki bala kuweka alama yoyote huku matengenezo ya barabara hiyo yakiendelea katik eneo hilo.

Aliongeza kuwa miili ya marehemu hao iliyokuwa imehalibika vibaya kutokana na kufumuka fuvu la kichwa cha aliyekua dereva wa pikipiki hiyo  na ubongo kusambaa katika eneo hilo imehifadhiwa katika hospital ya mkoa.

No comments:

Post a Comment