Linapokuja suala la kuhakikisha mama wa mwanae, North anapendeza
kadri iwezekanavyo, Yeezy hana mkono wa birika. Na ndio maana ametema
$250,000 (zaidi ya shilingi milioni 400) kwaajili ya kundi la watu
wanaompamba Kim Kardashian ( glam squad).
Staa huyo amekuwa akisindikizwa na mchumba wake kwenye ziara yake Yeezus
nchini Marekani na amehakikisha mtu wa kumpamba nywele Kim (hair
dresser) msanii wa make-up na mtu wa mitindo kuitwa muda wowote na
mahali popote wanapohitajika kumpamba mrembo huyo kwakuwa amekataa
kutumia watu wengine.
Chanzo kimeuambia mtandao wa RadarOnline.com: ‘Kanye amemuambia Kim
atatumia kiasi chochote kuufanya muonekano wake tayari kwa upigaji picha
mkubwa muda wowote akitaka Hivyo hair stylist wa Kim, make-up artist na
mtu wa mitindo wote wanaoishi Los Angeles, wako tayari saa 24/7,
kuchukua private jet kumfuata alipo.
“Kim anaamini timu yake pekee kumfanya apendeze na hataki kufanya
kazi na watu wa nje. Hii si rahisi na Kanye ametoa $250,000 wakati yupo
kwenye ziara kwaajili hiyo. Pesa haina maana yoyote kwa Kanye sababu
anataka mrembo wake aonekane bomba,” kilisema chanzo hicho.
Inadaiwa kuwa Kanye hachukizwi na matumizi makubwa ya Kim sababu yeye mwenyewe hutumia fedha nyingi mno kwaajili yake.
No comments:
Post a Comment