Kwa watumiaji wa Instagram, umeshawahi kuwa na picha unayohitaji
kushare na mtu flani peke yake bila marafiki wengine kuiona, lakini
ukashindwa kutokana na kutokuwa na huduma hiyo hapo awali? Instagram
wameligundua hilo.
Mtandao wa Instagram unaozidi kukua kwa kasi jana alhamisi (Dec 12)
umetangaza kipengele kipya kwa watumiaji wake, ambao sasa wanaweza
kutumiana picha, video na ujumbe moja kwa moja ‘Instagram Direct’.
Hapo Kabla mtumiaji wa Instagram alikuwa na uwezo wa kushare tu picha
ambayo inaonekana kwa followers wake wote hivyo haikuwa na privacy,
lakini kwa kipengele kipya cha ‘Instagram Direct’ mtu anaweza kuwatumia
picha na video watu anaowataka kuanzia mtu mmoja hadi 15 na ni private.
“Wakati mwingine unahitaji kushare sio na kila mtu, lakini na kundi
flani maalum” alisema Co-founder na chief executive wa Instagram Kevin
Systrom , wakati wa utambulisho wa feature hiyo jijini New York jana.
No comments:
Post a Comment