Habari ya ‘mujini’ Nairobi ni kuwa mwimbaji wa Kenya Avril
Nyambura sasa ni mchumba wa mfanyabiashara tajiri wa Afrika Kusini
ambaye ndiye anategemea kumuoa mwakani.
Baada ya taarifa juu ya kuchumbiwa kwa mrembo huyo wa Ogopa Djs ya
Kenya kusambaa wiki chache zilizopita, Avril amekanusha uvumi ulioenea
kuwa yuko kwenye uhusiano na mfanya biashara huyo kwasababu ya pesa.
“Tumefahamiana muda mrefu, kama ni kuhusu pesa ningekuwa naendesha
Range Rover mwaka huu na nisingekuwa naishi South B. He is amazing,
tunaelewana na sijali kile watu wasemacho”, alisema muimbaji wa Hakuna
Yule, Avril.
Avrila amesema ndoa yao haitakuwa hivi karibuni kutokana na wao wote
kutoka makabila tofauti mchumba wake ni Mzulu na Avril ni Mkikuyu,
hivyo kuna taratibu za kitamaduni za kufuata “The wedding won’t be that
soon. He is Zulu and I am Kikuyu, there are some cultural things
involved,”.
Kwa sasa Avril na mumewe mtarajiwa wako Mombasa kwaajili ya
kusheherekea Christmas, na baadaye wataelekea Johannesburg kwaajili ya
kuupokea mwaka mpya.
No comments:
Post a Comment